• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Majaliwa ampa siku 15 mkandarasi kukamilisha miradi ya barabara

by bajeti
October 21, 2022
in Habari
0
Majaliwa:Viongozi fuateni falsafa ya Serikali kuhudumia wananchi

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,DODOMA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa siku 15  kwa Kampuni ya Inter Country Contractors kuhakikisha inakamilisha ujenzi wa miradi ya barabara katika Kisiwa cha Ukerewe mkoani Mwanza.

Majaliwa ametoa agizo hilo  Oktoba 20, 2022 ofisini kwake jijini Dodoma wakati alipokutana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR TAMISEMI) Angellah Kairuki pamoja na Viongozi wa Wilaya ya Ukerewe na Watendaji wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini  (TARURA).

Amesema kampuni hiyo ilipewa kandarasi ya ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 13 kwa kiwango cha lami na changarawe katika kisiwa hicho ambapo ilipaswa kukamilisha kazi hiyo mwezi Julai mwaka huu.

“Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan inatoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa barabara, katika hili tumetoa kipaumbele kwa wakandarasi wazawa, tunachotegemea ni uaminifu wenu na utekelezaji wa miradi hii iwe ya viwango na mkamilishe kwa wakati”amesema Majaliwa

Aidha Majaliwa ameongeza kuwa ni vyema Mameneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mjini (TARURA) Mikoa na Wilaya wakatekeleza majukumu yao ipasavyo ili kuhakikisha ujenzi wa barabara katika maeneo mbalimbali nchini na ukamilika kwa wakati na kwa viwango vilivyokusudiwa.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Angellah Kairuki amesema wamepokea maelekezo ya Waziri Mkuu na kuahidi kufanya mapitio makubwa ya mfumo wa kiutendaji wa TARURA ili kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa miradi ndani ya taasisi hiyo.

Next Post
Serikali yawaonya Wakadiriaji Thamani za Ardhi na Mali

Serikali yawaonya Wakadiriaji Thamani za Ardhi na Mali

Masanja:Onesho la SITE kufungua fursa ya Utalii Dar es Salaam

Masanja:Onesho la SITE kufungua fursa ya Utalii Dar es Salaam

Taasisi ya Jai yaomba gharama za matibabu ya figo kupunguzwa

Taasisi ya Jai yaomba gharama za matibabu ya figo kupunguzwa

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:17
  • Today's page views 17
  • Total visitors 13,276
  • Total page views 15,024

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In