NA MIRIAM SARAKIKYA,ARUSHA.
WAZIRI wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Anjelina Mabula amesema Serikali itawachukulia hatua za kinidhamu wathamini wote watakaobainika kukiuka maadili ya taaluma zao.
Waziri Mabula ametoa kauli hiyo Oktoba 20,2022 mkoani Arusha wakati akifungua Mkutano Mkuu wa tatu wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Thamani wenye kauli mbiu isemayo ‘uthamini kichocheo cha uwekezaji’
Mabula amesema wapo wathamini wachache wanao chafua taaluma hiyo hivyo serikali inahitaji kufanya kazi na wafanyakazi waadilifu na wenye kusaidia kuleta maendele ya nchi na mtu mmoja mmoja
Aidha amefafanua kuwa Wakadiriaji wa Thamani za Ardhi na Mali wanatakiwa kufanya vizuri katika kazi zao kwani wasipofanya hivyo watasababisha hasara ya kutofikiwa kwa malengo ya mwekezaji mmoja mmoja, taasisi na Taifa kwa ujumla na kuitaka Bodi ya Usajili wa Thamani nchini kutambua thamani za Ardhi katika maeneo mbali mbali nchini .
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wathamini nchini Cletus Ndjovu amebainisha kuwa tayari bodi hiyo imeshamchukulia hatua mmoja wa wathamini
“Kutokana na utovu wa nidhamu Mthamini mmoja amefungiwa huku kampuni za usajili tano zimepigwa faini kwa viwango mbalimbali na wathamini watatu wamepewa onyo”ameeleza Ndjovu




Discussion about this post