• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Dkt.Mpango:Tanzania ni sehemu sahihi ya kuwekeza

by bajeti
November 5, 2022
in Mazingira
0
Dkt.Mpango:Tanzania ni sehemu sahihi ya kuwekeza

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wawekezaji mara baada ya majadiliano baina ya Tanzania, wawekezaji na wawakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kuhusu Mradi wa Umwagiliaji wa Bonde la Mara,majadiliano yaliofanyika katika Jukwaa la Uwekezaji Barani Afrika linalofanyika Jijini Abidjan nchini Ivory Coast.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Share on FacebookShare on Twitter

IBIDJAN,IVORY COAST

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango ameongoza majadiliano ya Tanzania na Wawekezaji mbalimbali wenye nia ya kuwekeza katika Mradi wa Umwagiliaji wa Bonde la Mara, majadiliano yaliofanyika katika Jukwaa la Uwekezaji Barani Afrika mwaka 2022 linalofanyika Jijini Abidjan nchini Ivory Coast.

Akizungumza katika majadiliano hayo, Makamu wa Rais Dkt.Mpango amesema Tanzania ni sehemu sahihi zaidi ya uwekezaji kusini mwa Jangwa la Sahara kwa kuwa ni lango muhimu zaidi kibiashara kwa nchi za Afrika Mashariki zenye watu zaidi ya milioni 300 pamoja  nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC) zenye watu zaidi ya milioni 450.

Amesema uwepo wa ardhi ya kutosha na hali ya hewa inayofaa kwa kilimo kikubwa pamoja na viwanda vya kusindika mazao ya kilimo inatoa ishara ya mazingira rafiki ya uwekezaji.

Dkt.Mpango amesema Tanzania  ina hekta milioni 44 zilizoainishwa kwaajili ya  kilimo, na takriban hekta milioni 10.8 pekee  zinazolimwa. Ameongeza kwamba  Eneo linalofaa kwa umwagiliaji linakadiriwa kuwa hekta milioni 29.4, na takriban asilimia 2.4 pekee zimetumika.

Pamoja na hayo, Makamu wa Rais ametaja juhudi mbalimbali zinazofanywa na serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan zenye lengo la kuboresha mazingira ya uwekezaji kama vile uboreshaji wa miundombinu ikiwemo reli na barabara, bandari, usafiri wa anga  pamoja na maboresho katika upatikanaji wa nishati ya uhakika.

“Licha ya janga la Uviko 19 miradi ya uwekezaji kutoka mataifa ya nje  iliosajiliwa  nchini Tanzania imeongezeka  mara tano zaidi hadi kufikia dola bilioni 2.2 mwaka 2021 kutoka dola milioni 454 mwaka 2020″amesema Dkt.Mpango

Awali akiwasilisha mradi huo kwa wawekezaji Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Raymond Mndolwa amesema mradi huo unatarajia kuimarisha miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji, ufugaji na uvuvi pamoja na kuongeza thamani ya mazao ya kilimo katika eneo hilo.

Aidha Mndolwa amesema mradi utaongeza kipato kwa wakulima wadogo wanaoishi maeneo hayo pamoja na kuongeza ajira na uzalishaji wenye tija.

Mradi wa Umwagiliaji wa Bonde la Mara unatarajiwa kutekelezwa katika wilaya ya Serengeti , Tarime na Butiama Mkoani Mara.

 

Next Post
Ukame waua Tembo 205, Nyumbu 512

Ukame waua Tembo 205, Nyumbu 512

Ukame

TaTEDO yahamasisha matumizi ya  jiko linalotumia joto kupikia badala ya moto kulinda mazingira.

TaTEDO yahamasisha matumizi ya jiko linalotumia joto kupikia badala ya moto kulinda mazingira.

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In