NA MIRIAM SARAKIKYA,ARUSHA
NAIBU Waziri wa Uwekezaji,Viwanda na Biashara Exaud Kigahe amewataka Wafanyabiashara nchini wakiwemo wa makampuni ya Ndege na Sekta ya Utalii kutumia teknolojia mbadala za kupunguza uchafuzi wa mazingira ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Kigahe ametoa kauli hiyo Desemba 5,2022 jijini Arusha wakati akizindua Maadhimisho ya Kitaifa ya Ushindani kwa mwaka 2022 jijini Arusha.
Amesema ni muhimu kwa wafanya biashara kutumia teknolojia za kisasa katika vyombo vya usafiri ili kuweza kutunza mazingira.
“Ilikupunguza ongezeko la mabadiliko ya tabia nchi naomba nitoe wito kwa makampuni kutumia teknolojia ili kutunza hewa safi ambayo ni rafiki pia kwa wanayama na binadamu “amesema Kigahe
Hata hivyo Kigahe ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini amebainisha kuwa ukataji wa miti hovyo umekuwa ukichangia uharibifu wa mazingira na kuongeza kuwa ni muhimu kwa wananchi wanaoishi pembezoni mwa hifadhi za wanyamapori kupunguza ukataji wa miti kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kijamii.
Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Mrisho Gambo amebainisha kuwa kuna haja ya kutolewa kwa elimu zaidi kwa wafanya biashara wadogo ili waweze kukuza soko kwa kuingia kwenye ushindani mkubwa wa kibiashara kwa mataifa mengine.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Ushindani (FCT) Jaji Salama Magimbi amefafanua kuwa Baraza hilo liliundwa kwa lengo la kudhibiti bidhaa bandia ili kukuza uchumi wa soko la Tanzania.
Katika Kilele cha maadhimisho hayo ambayo kitaifa yamefanyika jijini Arusha huku kaulimbiu ikiwa ni ‘Ushindani wa Utalii Endelevu’ lengo likiwa ni kuboresha Utalii hususani katika kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi.




Discussion about this post