• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Masanja:TAWA fanyeni kazi kwa ushirikiano kufikia malengo

by bajeti
December 19, 2022
in Habari
0
Masanja:TAWA fanyeni kazi kwa ushirikiano kufikia malengo

Kaimu Kamishna wa Uhifadhi, Mabula Misungwi (kushoto) akimkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mary Masanja (katikati) kuzungumza na Menejimenti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) inayoendelea na mafunzo ya uongozi katika Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Pasiansi jijini Mwanza Desemba 19,2022.Kulia ni Naibu Kamishna wa Uhifadhi- Huduma za Shirika, Prosper Kisima.(Picha na Wizara ya Maliasili na Utalii)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWADISHI WETU,MWANZA

NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja ameitaka menejimenti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuiwezesha kutimiza malengo yaliyowekwa.

Masanja ametoa kauli hiyo Desemba 19,2022 jijini Mwanza mara baada ya kuitembelea Menejimenti ya TAWA inayoendelea na mafunzo ya uongozi katika Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Pasiansi.

Masanja ameongeza kuwa utendaji kazi wenye kuzingatia ushirikiano na upendo ni nguzo muhimu itakayowawezesha kurekebishana na kukosoana kiutendaji kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa.

Aidha, amesisitiza kuwa ni vyema menejimenti hiyo ikajiwekea utaratibu wa kujadili changamoto mbalimbali pamoja ili iweze kufika mbali kiutendaji.

“Mwenzako anapokutana na changamoto yoyote ichukulie kama ni yako,tunahitaji tufanikiwe kwa kutatua changamoto zinazotukabili kwa pamoja ” amesisitiza Masanja.

Mafunzo hayo yenye lengo la kuwajengea uwezo viongozi  katika usimamizi wa masuala mbalimbali yakiwemo ya rasilimali watu, fedha na taratibu za manunuzi yametolewa kwa Manaibu Kamishna, Makamanda wa Kanda, Makamishna Wasaidizi Wandamizi na Makamishna Wasaidizi.

 

Next Post
NEPAL

NEPAL

Mpango wa jamii kukabili athari za mabadiliko ya tabianchi waja nchini.

Mpango wa jamii kukabili athari za mabadiliko ya tabianchi waja nchini.

Senyamule:Anachokifanya Rais Samia ni kwa ajili ya watanzania wote

Senyamule:Anachokifanya Rais Samia ni kwa ajili ya watanzania wote

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In