YAOUNDE,CAMEROON
WAKATI Dunia ikiomboleza vifo vya watu zaidi ya 47,000 vilivyotokana na tetemeko la ardhi nchini Uturuki na Syria matatizo ya kimazingira yanaendelea kuikumba sayari ya Dunia katika maeneo tofauti ambapo nchini Cameroon vumbi kutoka Jangwa la Sahara limeikumba nusu ya nchi hiyo.
Wakati hayo yakijiri vimbunga,ukame,mafuriko,ongezeko la joto pamoja na kuongezekana kwa maji ya bahari limekuwa jambo la kawaida kutangazwa na kusabisha vifo vya maelfu ya watu duniani lakini vumbi kusambaa nusu ya nchi limeonekana kuwa ni tofati na majanga mengine yanayoikumba dunia
Hata hivyo katika hali isiyokuwa ya kawaida nchini Cameroon kumekuwa na vumbi la ajabu hali iliyosababisha serikali kutoa tahadhari juu ya janga hilo ambalo ni nadra kutokea duniani
Awali Februari 16,2023 Waziri wa Uchukuzi wa Cameroon Ernest Ngalle Bibehe amesema kiwango kikubwa cha vumbi kutoka Jangwa la Sahara kinatarajiwa kuathiri nusu ya Cameroon.
Bibehe, ameonya kuwa vumbi hilo linaweza kusababisha ajali za barabarani kutokana na kupunguza uwezo wa madereva kuona mbali na kusababisha matatizo ya kupumua.
Hata hivyo vumbi kubwa linaendelea kushuhudiwa nchini humo kwa sasa katika eneo la Kaskazini mwa nchi hiyo na huenda likaathiri maeneo mengine na kutolewa tahadhari ikiwataka watu kuendesha magari kwa umakini na kufunika macho pamoja na pua.
Cameroon inadaiwa kushuhudia kiwango kikubwa cha vumbi kutoka Jangwa la Sahara kila mwaka, hasa sehemu za Kaskazini na Kusini.



Discussion about this post