• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Wafugaji wapewa madume bora 366 ya ng’ombe kuboresha mifugo yao

by bajeti
April 8, 2023
in Habari
0
Wafugaji wapewa madume bora 366 ya ng’ombe kuboresha mifugo yao

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akikagua madume bora ya ng’ombe yaliyogawiwa kwa vikundi vya wafugaji katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Mkoani Singida Aprili 6, 2023.(Picha na mpigapicha wetu)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MBARAKA KAMBONA,SINGIDA

RAIS Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa kiasi cha Sh. Milioni 878. 4 kwa ajili ya  kununua  madume bora 366 ya ng’ombe ili wafugaji waweze kuboresha mifugo yao.

Madume hayo yatawawezesha wafugaji kuwa na ng’ombe chotara ambao wanauwezo wa kuzalisha wastani wa kilo 150- 200 za nyama ukilinganisha na uzalishaji wa kilo 80-120 kwa Ng’ombe wa asili

Hayo yamezungumzwa Aprili 6,2023 na Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega wakati wa hafla ya kugawa madume bora 40 kwa vikundi vya wafugaji iliyofanyika  katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama mkoani Singida.

Amesema ni kwa wafugaji kujua  kuwa soko la nyama inayozalishwa hapa nchini limefunguka hivyo wajipange kubadilika na kufanya ufugaji wa kibiashara ili waweze kuongeza tija katika uzalishaji.

“Ndio maana Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa kiasi cha Sh. Milioni 878. 4 kwa ajili ya  kununua haya madume bora 366 ili wafugaji tuweze kuboresha mifugo yetu, tuweze kupata ng’ombe wanaoweza kutoa nyama nyingi na kufanya biashara yenye tija kuliko hivi sasa.

“Mifugo ni uchumi, na leo nawaambieni nyama ni dili, Rais Samia amefungua milango, wakati huu tunapokea wageni wengi kutoka nje ya nchi wakitaka kufanya biashara ya nyama na nchi yetu”amesema Ulega

Naye, Mbunge wa Iramba Mashariki, Francis Mtinga amemshukuru Waziri Ulega kwa kuwezesha wafugaji wa Wilaya ya Mkalama kupata madume bora 40 na kuahidi kuyatumia vizuri madume hayo kuboresha uzalishaji wa mifugo yao.

Halmashauri ambazo zimepata mgao huo ni pamoja na Mkuranga 50, Mvomero 40, Buchosa 46, Chamwino 50, Maswa 50, Chato 50, Msalala 50 na Mkalama 40.

 

Next Post
COSTECH yatoa Sh.Milioni 250 kwa mbunifu wa mita za maji kuanzisha kiwanda.

COSTECH yatoa Sh.Milioni 250 kwa mbunifu wa mita za maji kuanzisha kiwanda.

Serikali,Wadau Sayansi na Teknolojia waombwa kusaidia bunifu ndogondogo

Serikali,Wadau Sayansi na Teknolojia waombwa kusaidia bunifu ndogondogo

CAG Kichere apendekeza Vyura wa Kihansi kurudishwa nchini kutoka Marekani

CAG Kichere apendekeza Vyura wa Kihansi kurudishwa nchini kutoka Marekani

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In