• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Biashara haramu ya wanyama na mimea pori yashika nafasi ya nne duniani

by bajeti
May 30, 2023
in Mazingira
0
Biashara haramu ya wanyama na mimea pori yashika nafasi ya nne duniani

Mwakilishi wa Taasisi ya Infonile nchini Tanzania Daniel Samson (mwenye fulana nyeupe)akimuonesha mwandishi wa habari jinsi ya kutumia zana ya WILDEYE katika kupata taarifa za uhalifu dhidi ya wanyamapori Mei 26,2023 jijini Dar es Salaam wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wanahabari juu ya masuala ya wanyamapori.(Picha na Infonile)

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO

BIASHARA haramu ya Viumbe na Mimea pori (Wildlife) imetajwa kushika nafasi ya nne duniani baada ya ile ya binadamu,dawa za kulevya na bidhaa feki ambapo imefikia kiasi cha dola za kimarekani Bilioni  23.

Hayo yameelezwa  Mei 26,2023 jijini Dar es Salaam  na Mtaalamu wa Masuala ya Wanyamapori  kutoka jijini Arusha Allen Mgaza wakati wa semina kwa waandishi wa habari juu ya uhalifu dhidi ya  wanyamapori  iliyoandaliwa  na Taasisi ya Infonile kutoka nchini Uganda.

Akizungumzia biashara hiyo,Mgaza amesema  biashara hiyo ni tishio kwa Taifa na kimataifa hivyo kunahitajika juhudi kubwa kwa kushirikiana na serikali ili kupambana na biashara hiyo ya viumbe pori licha ya kuwa baadhi ya biashara hiyo inafanywa kihalali.

Amesema wafanyabishara haramu wa viumbe na mimea pori hutumia njia mbalimbali za kificho katika kusafirisha malighafi hizo ili wasiweze kugundulika

 “Masuala ya tibaasili yanachangia kuwepo kwa biashara hiyo kutokana na kuwepo kwa mimea inayovunwa kwa ajili ya dawa.

“Kuna ndege aina ya Tumbusi ambao wao hula mizoga ya wanyamapori hivyo kuna watu wanaimani kuwa wakipata kichwa cha ndege huyo basi watafanikiwa zaidi hivyo kufanya kila jitihada ili kuwauwa na kuchukua vichwa vyao.

“Sababu nyingine ya kuwepo kwa biashara hiyo ni kutumika kama chakula,kutengeneza vipodozi,kukamata wanyama kwa ajili ya kuwafunga binafsi na mwisho ni sababu za kisayansi”amesema Mgaza

Aidha ameongeza kuwa fedha zinazopatikana kutokana biashara hiyo zinadaiwa kutumika katika kufadhili makundi ya kigaidi,kuongeza rushwa na wakati mwingine ni hatari kwa kusababisha magonjwa yanayouwa watu wengi kama ebola na mafua ya ndege.

“Kuna umuhimu mkubwa wa kupambana na biashara hii hatari ambapo ikiwa haitadhibitiwa basi vizazi vijavyo havitaweza kuwaona tena wanyama na mimea pori”amesema Mgaza

Kwa upande wake Mwakilishi wa Taasisi ya Infonile nchini Daniel Samson amebainisha kuwa waandishi wa habari wanaweza kusaidia katika kukabiliana na biashara hiyo kwa kufichua na kuandika habari na mazingira yanayopeleka uwepo wake

“Waandishi wa habari waendelee kutumia zana kama WILDEYE katika kuwasaidia kupata taarifa za uhalifu dhidi ya wanyamapori nchini na nje ya nchi ndio maana Infoline iliamua kuandaa warsha ya kuwakutanisha waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali ili kuwajengea uwezo juu ya uhalifu dhidi ya wanyamapori na faida zake ikiwa watalindwa”amesema Samson

 

Next Post
Serikali kuwapa mikopo vijana waliojifunza uvuvi na ukuzaji viumbe maji

Serikali kuwapa mikopo vijana waliojifunza uvuvi na ukuzaji viumbe maji

Mazungumzo Burundi

Mazungumzo Burundi

“Lima chakula sio tumbaku.” huua watu milioni nane kwa mwaka

“Lima chakula sio tumbaku.” huua watu milioni nane kwa mwaka

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 13,062
  • Total page views 14,807

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In