• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

CCM:Wasomi fanyeni utafiti miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali

by bajeti
June 16, 2023
in Habari
0
CCM:Wasomi fanyeni utafiti miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,ZANZIBAR.

KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi na Uenezi Zanzibar Khamis Mbeto Khamis,amewasihi wasomi nchini kufanya utafiti wa kina wa kufuatilia na kutathmini kitaalamu miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ili wananchi wajue mafanikio hayo.

Mbeto ametoa kauli  hiyo  Juni 16,2023 Visiwani Zanzibar katika kongamano la kumpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Mwinyi, la kuelekea miaka mitatu ya uongozi wake  ambalo liliandaliwa na Tawi la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Kusini Unguja.

Ameeleza kuwa utafiti huo utawasaidia wananchi kuepuka upotoshaji unaofanywa kwa sasa na baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani kupitia mikutano yao ya hadhara iliyofanyika kisiwani Pemba.

Mbeto, ameongeza kuwa Zanzibar imepiga hatua kubwa za kimaendeleo chini ya uongozi wa Dk.Mwinyi,hivyo wanasiasa na viongozi wa upinzani wanatakiwa kuthamini na kuunga mkono juhudi hizo badala ya kubeza na kupuuza kwani nao ni miongoni mwa wanufaika wa maendeleo hayo.

“Wasomi msikubali kudanganywa fanyeni utafiti juu ya kazi kubwa iliyofanywa na Dk.Mwinyi toka aingie madarakani mpaka sasa, leteni majibu na kuibua hoja makini za kujenga mshikamano na maridhiano ya kisiasa yanayohimiza ukuaji wa uchumi wa nchi.

“Wapinzani  tunajua hawawezi kumpongeza wala kusifu juhudi hizo lakini japo mthamini na kuheshimu mamlaka za kiutawala,kwani nanyi ni wananufaika juu ya maendeleo hayo kwani ruzuku,mishahara na huduma zote muhimu za kibinadamu zinazofanywa na Serikali nanyi mnapata kama wananchi wengine”,amesema Mbeto.

Mbeto,amebainisha  kuwa Serikali ya awamu ya nane chini ya Uongozi wa Dk.Hussein Ali Mwinyi, inatekeleza kwa ufanisi Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 katika sekta mbalimbali nchini.

“Miaka mitatu ya uongozi wa Rais Dk.Mwinyi, tayari amejenga Shule za kisasa kuanzia ngazi za msingi hadi Vyuo Vikuu ili vijana wasome katika mazingira rafiki yanayoendana na mahitaji ya kitaaluma.

“Katika kuimarisha Uchumi wa nchi serikali imefungua milango ya uwekezaji kwa kusajili miradi mbalimbali ya maendeleo itakayojenga mahoteli makubwa ya kitalii ikiwemo kuimarisha sekta mbalimbali za miundombinu,Afya,Elimu, Anga,Nchi kavu na baharini,Utalii,Uwezeshaji Wananchi kiuchumi,Ustawi wa Jamii na kuweka Mazingira rafiki katika Uchumi wa buluu”amebainisha Mbeto

Mbeto, amewasihi wananchi wasikubali kupotoshwa kwani nchi ipo salama na inapiga hatua kubwa katika nyanja za  kiuchumi,kijamii,kisiasa,kiutamaduni na michezo nan kasi ya utendaji wa Serikali hiyo ya awamu ya nane imekuwa ni tishio kwa vyama vya upinzani nchini  hali inayosababisha waanze kuchanganyikiwa na kutoa hoja dhaifu.

 

 

Next Post
Google yaipongeza bajeti.co.tz

Google yaipongeza bajeti.co.tz

Finland kuzinyima misaada nchi za kiafrika zilizogoma kuipinga Urusi

Finland kuzinyima misaada nchi za kiafrika zilizogoma kuipinga Urusi

Mradi Kituo cha Utafutaji na Uokoaji Ziwa Victoria kati ya Tanzania na Uganda,viongozi wafanyia shughuli zao Kenya

Mradi Kituo cha Utafutaji na Uokoaji Ziwa Victoria kati ya Tanzania na Uganda,viongozi wafanyia shughuli zao Kenya

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In