NA MWANDISHI WETU
KAMPUNI ya Google kutoka nchini Marekani imetambua mchango unaotolewa na tovuti ya habari ya BAJETI.CO.TZ baada ya kuitunuku cheti cha hongera kutokana na watu wengi kuifuatilia bila kupewa kiunganisho(link) kupata taarifa zake .
Bajeti.co.tz inayochapisha taarifa zake kutoka jijini Dar es Salam nchini Tanzania-Afrika Mashariki imekuwa ikifuatilia na maelfu ya watu kutoka pembe mbalimbali za dunia kutokana na usahihi wa taarifa zake.
Akizungumzia jijini Dar es Salaam Juni 16,2023 mara baada ya kupokea cheti hicho,Mkurugenzi wa Bajeti Communication inayoendesha tovuti hiyo, Goodluck Hongo amesema ni jambo la furaha kuona Kampuni kubwa duniani kama Google kuitunuku cheti cha hongera tovuti yao ya BAJETI.CO.TZ kwa kuvuka viwango ilivyoweka.
“Mimi na timu nzima ya BAJETI COMMUNICATION tumefurahi sana kupokea cheti cha hongera kutoka Kampuni maarufu duniani ya Google kwa kutuona sisi BAJETI bila kuwepo kwa upendeleo kwa kuwa wanaotumia huduma za Google ni watu wote duniani.
“Tunawashukuru Google kwa zawadi hii,tunasema asante sana Google na hongera hizi itakuwa ni chachu kwetu kuongeza juhudi zaidi za kazi ili dunia iendelee kuitumia Bajeti.co.tz kama chanzo cha taarifa sahihi zenye kujenga,kuelimisha, na wakati mwingine kuhimiza amani ili dunia iwe sehemu salama ya kuishi lakini pia ni hongera za watanzania wote na nchi yetu Tanzania.
“Kutokana na hongera hizi tunafikiria kuweka pia na mfumo wa lugha zingine kama Kiingereza ili wale wasiojua Kiswahili basi watasoma kwa lugha zingine”amesema Hongo
Bajeti.co.tz ni tovuti ya habari iliyochini ya Bajeti Communication yenye makao yake makuu jijini Dar es Salaam nchini Tanzania,Afrika Mashariki ambayo hutoa taarifa zake kwa lugha ya Kiswahili.




Discussion about this post