• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Putin:Tutailinda nchi yetu dhidi ya uhaini

by bajeti
June 24, 2023
in Habari
0
Putin:Tutailinda nchi yetu dhidi ya uhaini

Rais wa Urusi Vladmir Putin

Share on FacebookShare on Twitter

MOSCOW,RUSSIA

MACHO ya dunia yameelekezwa nchini Urusi baada ya Kiongozi wa Kampuni binafsi ya Kijeshi Wagner Group Evgeny Prigozhin kuasi na kuapa kupambana na majeshi ya Urusi wakati nchi hiyo ikiwa katika oparesheni yake ya kijeshi dhidi ya Ukraine iliyoianzisha Februari 24,2022.

Hata hivyo Rais wa Urusi Vladmir Putin amesema jaribio la mapinduzi lililofanywa na Prigozhin ni uhaini na kwamba wanauzoefu wa hali kama hizo na watailinda nchi yao dhidi ya uhaini.

Wakati Rais Putin kauli hiyo ,usalama unaidaiwa kuimarishwa jijini Moscow na maeneo mengine ya Urusi huku vikosi vya jeshi la nchi hiyo vikishambulia magari ya msafara wa Kiongozi wa Kampuni Binafsi ya Kijeshi ya Wagner Group Evgeny Prigozhin

Rais Putin ametoa hotuba hiyo kwa taifa Juni 24,2023 jijini Moscow muda mfupi baada ya vikosi vya Prigozhin kuvuka mpaka kutoka Ukraine walikokuwa wakipigana na kisha kuliteka jiji la Rostov-on-Don kusini mwa Urusi.

Amesema jaribio la uasi lililofanywa na mkuu wa kampuni ya kijeshi ya kibinafsi ya Wagner, Evgeny Prigozhin, ni sawa na usaliti kwa Urusi na watu wake na kuapa kwamba vyombo vya kutekeleza sheria nchini vitachukua hatua madhubuti kurejesha utulivu.

Alibainisha kuwa Moscow inahusika katika mapambano ya kihistoria ya kulinda mustakabali wake huku “ikizuia uchokozi kutoka kwa Wanazi mamboleo na mahasimu wao kutoka katika nchi za Magharibi.

“Tunapigania maisha na usalama wa watu wetu, uhuru na uhuru wetu,kwa haki ya kuwa na kubaki Urusi na kwamba vikosi vya Wanajeshi vya Urusi na mashirika mengine ya serikali yamepokea maagizo muhimu na hatua madhubuti zitachukuliwa ili kuleta utulivu katika Rostov-on-Don,” kusini mwa Urusi”amesema Rais Putin

Kiongozi wa Kampuni binafsi ya Kijeshi Wagner Group Evgeny Prigozhin

Wakati huo Idara ya Usalama wa Taifa (FSB)imefungua kesi ya jinai dhidi ya Prigozhin, kwa madai ya kutetea uasi dhidi ya serikali.

Awali, Wizara ya Ulinzi ya Urusi ilishumtumu Prigozhin kwa kueneza uwongo juu ya video iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii iliyodai kuwa jeshi la Urusi lilishambulia kambi ya wapiganaji wa Wagner.

Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu ilisema kwamba uhalifu huo unaweza kuadhibiwa kwa kifungo cha miaka 12 hadi 20.”

Hata hivyo ikiwa vikosi vya Urusi vitafanikiwa kuzima jaribio hilo na kuchukua uthibiti wa  jiji la Rostov-on-Don kusini mwa nchi itadhihirisha uwezo wake wa kijeshi.

 

Next Post
Wabunifu waishukuru Serikali kuwapatia Sh.Bilioni 1.191

Wabunifu waishukuru Serikali kuwapatia Sh.Bilioni 1.191

“Nyumbu na Tembo vinara kutumia shoroba”

"Nyumbu na Tembo vinara kutumia shoroba"

Urusi yaichanganya dunia,EU yasema sasa ni hatari zaidi kuliko awali

Urusi yaichanganya dunia,EU yasema sasa ni hatari zaidi kuliko awali

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:5
  • Today's page views 5
  • Total visitors 13,061
  • Total page views 14,806

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In