• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Sayansi na Teknolojia

Serikali kuimarisha teknolojia ya anga za juu

by bajeti
June 30, 2023
in Sayansi na Teknolojia
0
Serikali kuimarisha teknolojia ya anga za juu

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

WAZIRI wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amefanya kikao na Shirika la Sayansi na Teknolojia la Anga la China (CASC) ikiwa ni sehemu ya mikakati ya Serikali katika kujenga na kukuza uchumi wa kidijitali.

Hata hivyo Nape aliongoza na  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maafisa kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Tume ya TEHAMA Tanzania (ICTC) na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na Shirika la habari la China (CRI)  Juni 28,2023 imeeleza kuwa CASC ni mkandarasi mkuu wa anga za juu wa China ambaye amefanya majaribio kadhaa yenye mafanikio ya kupeleka chombo cha anga za juu kama sehemu ya mipango ya kukusanya sampuli za asteroid na kuzileta salama duniani.

Hata hivyo CRI ilimnukuu Waziri Nape akisema kwa ufupi baada ya mkutano huo  kuwa pande hizo mbili zinalenga kuimarisha ushirikiano katika teknolojia ya anga ya juu na ulinzi wa taarifa binafsi.

“Hii ni sehemu ya mikakati ya serikali katika kujenga na kukuza uchumi wa kidijitali ambao utatoa maisha bora kwa Watanzania kupitia TEHAMA,” amesema Nape

Hatua hiyo mpya imekuja kufuatia uamuzi wa China wa kupanua sera yake ya diplomasia ya anga ya juu kwa kuzikaribisha nchi mbalimbali hasa nchi za Afrika kuchangamkia fursa zinazopatikana katika uchunguzi wa anga, kuboresha sayansi na kuzalisha wanaanga wengi.

 

Next Post
Mwanamfalme Harry wa Uingereza apokonywa  nyumba baada ya  kuikosoa familia yake

Mwanamfalme Harry wa Uingereza apokonywa nyumba baada ya kuikosoa familia yake

Shoroba zifunguliwe kupunguza athari za  wanyamapori wakali na waharibifu

Shoroba zifunguliwe kupunguza athari za wanyamapori wakali na waharibifu

Dkt.Mpango aitaka JKT kuwekeza matumizi ya teknolojia

Dkt.Mpango aitaka JKT kuwekeza matumizi ya teknolojia

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In