• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Serikali yaandaa mwongozo Uingizaji, Matumizi na Utupaji Salama wa Zebaki.

by bajeti
August 23, 2023
in Mazingira
0
Serikali yaandaa mwongozo Uingizaji, Matumizi na Utupaji Salama wa Zebaki.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira pamoja na watalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais wakiwa katika kikao cha kupokea taarifa ya hatua zilizofikiwa juu ya uratibu na utekelezaji wa Mpango-kazi wa Taifa wa Kupunguza Matumizi ya Zebaki (2020 - 2025) iliyowasilishwa na Ofisi ya Makamu wa Rais jijini Dodoma Agosti 22, 2023.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

SERIKALI kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imeandaa Mwongozo wa Uingizaji, Matumizi na Utupaji Salama wa Zebaki.

Hayo yamezungunzwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Khamis Hamza Khamis Agosti 22,2023 jijini Dodoma wakati akiwasilisha taarifa ya hatua zilizofikiwa juu ya uratibu na utekelezaji wa Mpango-kazi wa Taifa wa Kupunguza Matumizi ya Zebaki (2020 – 2025) kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira.

Amebainisha kuwa Mwongozo huo unalenga kutoa utaratibu wa njia salama za usimamizi wa Zebaki pasipo kuathiri afya ya binadamu na mazingira.

Hata hivyo amesema utafiti walioufanya kuhusu teknolojia mbadala wa zebaki kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu nchini umeonesha kuwa teknolojia za kuchoma (smelting) kwa kutumia borax na teknolojia za sianadi (cyanidation) ndio zinatumika kwa wingi nchini na nchi zinazoendelea.

Khamis ameongeza kuwa Mradi wa Kudhibiti Athari za Zebaki kwa Afya ya Binadamu na Mazingira Kwenye Shughuli za Uchimbaji Mdogo wa Dhahabu Nchini umejikita katika kufanyia kazi teknolojia zinazotumika zaidi nchini.

”Lengo ni kutekeleza malengo la Mkataba wa Minamata hususan kipengele cha saba kinachohusu kupunguza matumizi ya zebaki kwenye uzalishaji wa dhahabu inayozalishwa na wachimbaji wadogo na pale itakapowezekana kuondoa kabisa matumizi ya kemikali hiyo katika kuzalisha dhahabu kwa wachimbaji wadogo,” amefafanua Khamis

Hata hivyo ametaja shughuli za mradi huo  kuwa ni kuimarisha na kujenga uwezo na ujuzi wa taasisi na wachimbaji wadogo kuhusu namna ya kudhibiti athari zinazotokana na utumiaji wa zebaki kwenye uzalishaji wa dhahabu.

Mradi huo wa miaka minne unafadhiliwa na Global Environmetal Facility (GEF) kwa ruzuku ya Sh.Bilioni 18.3 ambapo unatekelezwa katika mikoa saba ya Geita, Mwanza, Mara, Shinyanga, Singida, Mbeya na Songwe.

Next Post
Maafisa Ununuzi na Ugavi wahimizwa kuzingatia sheria

Maafisa Ununuzi na Ugavi wahimizwa kuzingatia sheria

Magonjwa yatajwa chanzo cha Mbwamwitu  kutoweka

Magonjwa yatajwa chanzo cha Mbwamwitu kutoweka

Mazungumzo

Mazungumzo

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In