• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Magonjwa yatajwa chanzo cha Mbwamwitu kutoweka

by bajeti
August 30, 2023
in Mazingira
0
Magonjwa yatajwa chanzo cha Mbwamwitu  kutoweka

Mbwamwitu wakiwa katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Agosti 26,2023 kutoka Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi.

Share on FacebookShare on Twitter

NA MIRIAM SARAKIKYA, ARUSHA

SERIKALI kupitia Taasisi  ya  Utafiti  Wanyamapori  Tanzania (TAWIRI)  na Hifadhi za Taifa Tanzania TANAPA)  zinaendelea  na zoezi endelevu la kuwarejesha Mbwa mwitu ndani  ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ikiwa ni kuhakikisha kuwa wanyamapori hao wanaendelea kuhifadhiwa katika mfumo _wa ikolojia_  ya Serengeti.

Hayo yamezungumzwa jijini  Arusha Agosti 29,2023 na Mtafiti Mkuu na Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti Serengeti Dkt. Emmanuel Masenga wakati wa zoezi la kuwapokea Mbwamwitu zaidi ya  20  waliotoka Hifadhi ya Taifa Mkomazi na kuhamishiwa  katika Hifadhi ya Taifa Serengeti kabla ya kuachiwa huru.

Dkt.Masenga amesema kuwa matokeo ya tafiti yanaonyesha kuwa sababu kuu za kutoweka kwa Mbwamwitu katika Hifadhi ya Serengeti ni magonjwa (Rabies and Canine Distemper Virus) na ongezeko la idadi ya Simba na Fisi ikiwemo kuuawa na wananchi wanapotoka nje ya hifadhi.

 

Aidha, Dkt. Masenga  amesema jitihada za Serikali  za kuwarejesha wanyamapori hao ndani ya Hifadhi ya Taifa Serengeti ni zoezi endelevu na lilianza tangu mwaka 2011 kwa lengo la kuwahifadhi  ili kutunza bioanuwai na kuendeleza utalii.

Dkt. Masenga  amebainisha kuwa kama inavyofahamika jukumu kubwa la Taasisi  ya  Utafiti  Wanyamapori  Tanzania (TAWIRI) ni kufanya  tafiti  za wanyamapori, hivyo TAWIRI  inaendelea kufanya tafiti za kina za kuhakikisha Mbwamwitu wanaendelea kuhifadhiwa katika mfumo ikolojia wa Serengeti

 

Next Post
Mazungumzo

Mazungumzo

Mahakama yasimama kwa muda kuhakiki kitambulisho cha mwandishi

Mahakama yasimama kwa muda kuhakiki kitambulisho cha mwandishi

Serikali kushirikiana na vyombo vya habari katika utoaji wa elimu ya mazingira

Serikali kushirikiana na vyombo vya habari katika utoaji wa elimu ya mazingira

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In