• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Mahakama yasimama kwa muda kuhakiki kitambulisho cha mwandishi

Ni baada ya wakili wa Damas Ndumbaro kuieleza mahakama kuwa kesi inayomhusu waziri haitakiwi kuripotiwa na vyombo vya habari

by bajeti
September 13, 2023
in Habari
0
Mahakama yasimama kwa muda kuhakiki kitambulisho cha mwandishi

Mahakama inayotembea

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

NAIBU Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi Mh.Crecensia Kisongo ameamuru mwadishi wa habari wa Bajeti Communication Goodluck Hongo kupelekwa mbele ya Ofisi ya Afisa Utumishi wa Mahakama hiyo ili iweze kuhakiki kitambulisho chake (press card) baada ya kutaka kuripoti kesi ya Rufaa namba 253/2022 inayomhusu Lydia Paulo Lugaga dhidi ya Damas Daniel  Ndumbaro.

Uamuzi huo umetolewa Septemba 11,2023 jijini Dar es Salaam wakati rufaa hiyo ilipoanza kusikilizwa muda mfupi baada ya Karani wa Mahakama kuwaita wahusika wa shauri hilo kwa kutumia kipaza sauti kama ilivyo utaratibu wa kila siku wa kuitwa kwa mashauri mbalimbali katika mahakama hiyo.

Mara baada ya kuingia katika chumba cha mahakama ,Wakili anayemtetea Damas Ndumbaro, Neema Masawe aliieleza  Mahakama hiyo kuwa kuna mtu aliyeingia ndani ya Mahakama hiyo ajitambulisha yeye ni nani ili ahafamike kabla ya kesi kuendelea.

Hata hivyo Hongo alijitambulisha mbele ya Naibu Msajili wa Mahakama hiyo Mhe.Kisongo kuwa yeye ni mwanahabari na yupo hapo kusikiliza na kuripoti shauri hilo,

Lakini  Masawe aliiambia Mahakama hiyo  kuwa kesi hiyo inamhusu Mheshimiwa Waziri hivyo haitakiwi kuripotiwa na vyombo vya habari.

“Mheshimiwa kesi hii inamhusu mheshimiwa Waziri hivyo haitakiwi kuripotiwa na vyombo vya habari,lakini hata hivyo ipo Chamber court”amesema Masawe

Mara baada ya kauli hiyo,Naibu Msajili Mfawidhi Kisongo alipitia kitambulisho cha mwandishi huyo na kisha kumwelekeza Karani wa Mahakama kuongozana naye hadi kwa Afisa Utumishi ili aweze kukihakiki.

“Peleka kwa Afisa Utumishi aweze kuhakiki hiki kitambulisho nawe mfuate huko”amesema Naibu Msajili Mfawidhi Kisongo

Hata hivyo Ofisi ya Afisa Utumishi ilikuwa imefungwa na badala yake Karani huyo alielekea katika Ofisi nyingine ya Afisa Utumishi ambayo ilikuwa na watu na baada ya kuonesha press card hiyo alishauriwa kumwambia  mwandishi huyo kuwa atoke nje na kisha kuwasubiri mawakili wa pande zote ndipo awahoji.

“Umeambiwa utoke nje kule chini na uwasubiri mawakili wote wakishatoka ndio uwahoji, nimeambiwa hivyo nikwambie”amesema Karani wa Mahakama hiyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana.

Akizungumza mara baada ya kuahirishwa kwa shauri hilo, Wakili upande wa mlalamikaji Pasensa Dickson amesema wapo hapo baada ya kupeleka Shauri la Rufaa la Mgogoro wa Ardhi  ambalo lilifunguliwa katika Baraza la Ardhi la Wilaya ya Ilala,

Amesema katika shauri hilo Lydia Lugaga alilalamika kuwa eneo lake lilivamiwa na Damas Daniel Ndumbaro ambapo alipeleka ushahidi wake wa jinsi alivyonunua eneo hilo na waliohusika kumsaidia kulipata kwa vielelezo lakini pia Damas Ndumbaro naye alipeleka ushahidi wake na ndiye aliyekuwa shahidi pekee kwa upande wake.

“Baada ya hapo Baraza lilitoa uamuzi wake ambao ulitupilia mbali madai ya Lydia lakini baada ya kufuatilia nakala ya hukumu na kuipitia upya niligundua kuwa kulikuwa na dosari kama nane yaliyonifanya tukate rufaa”

“Baada ya rufaa tulipangiwa Naibu Msajili Mfawidhi Kisongo ili ianze kusikilizwa lakini ilichelewa kutokana na  wakili upande wa utetezi kutokufika mahakamani kutokana na sababu mbalimbali ambazo Mahakama iliambiwa”amesema Dickson

Dickson ameongeza kuwa  kwa sasa Mahakama imeamua kesi hiyo isikilizwe kwa njia ya maandishi badala ya ile ya kawaida ambapo taratibu hizo zitaendelea tena mwezi Oktoba,2023

“Awali sisi tulipinga kesi hiyo kusikilizwa kwa maandishi lakini sasa imeamriwa tutaisikiliza kesi hiyo kwa njia ya maandishi,basi sisi tutafanya hivyo kama sheria inavyotaka na kisha Mahakama itapitia na itatoa uamuzi wake”amesema Dickson

Akizungumzia tukio la mwandishi, kufikishwa kwa Ofisa Utumishi,Afisa Uhusiano wa Mahakama hiyo Vicent Tiganya amesema wao wanafuatilia kujua hali ilivyokuwa na kwamba watamjulisha mwandishi juu ya hatua waliyofikia

“Nipo safarini Morogoro lakini nimelipokea na nitakupigia simu,nitakujulisha”amesema Tiganya

 

Next Post
Serikali kushirikiana na vyombo vya habari katika utoaji wa elimu ya mazingira

Serikali kushirikiana na vyombo vya habari katika utoaji wa elimu ya mazingira

Soko la Samaki Feri laelemewa na wafanyabishara

Soko la Samaki Feri laelemewa na wafanyabishara

Elimu kwa wanafunzi

Elimu kwa wanafunzi

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In