• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

UNEP kuendelea kufadhili miradi ya mazingira Tanzania

by bajeti
November 23, 2023
in Mazingira
0
UNEP kuendelea kufadhili miradi ya mazingira Tanzania

1. Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais,Mary Maganga akizungumza na Meneja Usimamizi wa Miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia kutoka Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), Dkt. Daniel Pouakouyou wakati wa kikao baina yao kilichofanyika katika Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma Novemba 22, 2023. Kikao hicho kililenga katika kujadili utekelezaji wa Mradi wa urejeshaji wa uoto wa asili na kuhifadhi bioanuai (SLR) na vipaumbele vipya vya miradi ya mazingira nchini (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Share on FacebookShare on Twitter

 

NA MWANDISHI WETU,DODOMA

MENEJA Usimamizi wa Miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia kutoka Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) Dkt. Daniel Pouakouyou amesema  UNEP itaendelea kuwa mshirika wa Tanzania katika ufadhili wa miradi ya mazingira.

Kauli hiyo ameitoa katika Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma Novemba 22, 2023 wakati alipofanya mazungumzo na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Mary Maganga

Mbali na hilo lakini pia viongozi hao wamejadili utekelezaji wa Mradi wa Urejeshaji wa Uoto wa Asili na Uhifadhi wa Bioanuai (SLR) na kufanya mapitio ya vipaumbele vya miradi mipya ya mazingira inayoandaliwa na Tanzania kwa kushirikiana na UNEP.

Dkt. Pouakouyou amesema UNEP itaendelea kuwa mshirika wa Tanzania katika ufadhili wa miradi ya mazingira ukiwemo mradi wa SLR unaotekelezwa katika Mikoa 5 nchini iliyopo katika Mabonde ya Mto Ruaha na Bonde la Ziwa Rukwa ikijumuisha wilaya za Iringa, Wanging’ombe, Mbarali, Mbeya, Sumbawanga, Tanganyika na Mpibwe.

Ameongeza kuwa lengo la ziara hiyo ni kuangalia vipaumbele vya miradi mipya ya mazingira inayofadhiliwa na UNEP na kuona maeneo mahsusi yanayohitaji ushirikiano wa karibu baina ya shirika hilo na Serikali ikiwemo upatikanaji wa fedha za utekelezaji wa miradi hiyo.

“Tunashukuru ushirikiano tunaendelea kuupata kutoka kwa Serikali. UNEP itaendelea  kufadhili miradi mipya ya mazingira ikiwemo mradi wa uhifadhi wa maeneo ya ardhi oevu katika mfumo ikolojia ya bonde la Mto Wami-Ruvu ambalo ni moja ya vyanzo vikuu cha maji kwa Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na maeneo ya jirani” amesema Dkt. Poukouyou.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Mary Maganga amemueleza Dkt. Poukouyou dhamira na juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali katika kukabiliana na athari za uharibifu wa mazingira na mabadiliko wa mazingira ikiwemo urejeshaji wa uoto wa asili katika maeneo mbalimbali ya nchi.

“Tunaishukuru UNEP kwa kuendelea kufadhili miradi ya mazingira hapa nchini, tumeandaa Mpango Kabambe wa Mazingira wa mwaka 2022-2032 ambapo moja ya maeneo ya kipaumbele ni pamoja na urejeshaji wa uoto wa asili, bioanuai na kuboresha hali ya mifumo-ikolojia na kujenga uwezo wa jamii kuwa na shughuli endelevu za uzalishaji” amesema  Maganga.

Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Wataalamu mbalimbali kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Ofisi akiwemo Mkurugenzi Msaidizi wa Mazingira Dkt. Paul Deogratius,Mratibu wa Kitaifa wa Mradi wa SLR, Dkt. Damas Mapunda na Afisa Mazingira Mwandamizi, Thomas Chali.

Next Post
Israel imeshindwa kuwapata mateka wake zaidi ya 200 waliotekwa na Hamas

Israel imeshindwa kuwapata mateka wake zaidi ya 200 waliotekwa na Hamas

Bajeti yaelemewa na vyeti vya pongezi kutoka Google

Bajeti yaelemewa na vyeti vya pongezi kutoka Google

COP 28,DUBAI

COP 28 Dubai-UAE

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In