• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Israel imeshindwa kuwapata mateka wake zaidi ya 200 waliotekwa na Hamas

Yakubali kusitisha mapigano,kubadilishana wafungwa

by bajeti
November 24, 2023
in Habari
0
Israel imeshindwa kuwapata mateka wake zaidi ya 200 waliotekwa na Hamas

Malori ya misaada yakielekea Ukanda wa Gaza.(Picha na Pars)

Share on FacebookShare on Twitter

GAZA,PALESTINA

KWA mara ya kwanza katika historia ya Dunia,Taifa la Israel lililokuwa likijulikana kama Taifa la Mungu kutokana na kuandikwa na kutabiriwa katika vitabu vya Dini hasa ya Kikristo limeshindwa vita dhidi ya Kundi la wapiganaji la Hamas kutoka Ukanda wa Gaza-Palestina.

Kushindwa huko kunakuja baada ya mapigano ya siku zaidi ya 40 tangu Israel ilipoanzisha mashambulizi ya kulipiza kisasi baada ya shambulio la Hamas ndani ya ardhi za Israel mnamo Oktoba 7,2023 licha ya Jeshi la Israel kulizingira eneo hilo kwa miaka zaidi ya 10.

Tangu kutokea kwa shambulio hilo viongozi mbalimbali wa nchi za Ulaya akiwemo Rais wa Marekani,Joe Biden walizuru Taifa la Israel ili kuliunga mkono kutokana na kitendo cha Hamas, kundi linalodaiwa kuungwa mkono na Iran ambalo linadaiwa kuwaua zaidi ya waisrael 1000 na wengine zaidi ya 200 kuwateka nyara.

Licha ya Israel kuwa na vikosi vya kisasa vyenye uwezo mkubwa katika vita,teknolojia na vifaa kikiwemo kikosi chake maarufu kama MOSSAD limeshindwa kuwapata mateka zaidi ya 200 waliotekwa katika uvamizi wa ajabu uliofanya na kundi la Hamas mnano Oktoba 7,2023 ndani ya ardhi za Israel.

Hata hivyo Israel ikisaidiwa na Nchi za Ulaya pamoja na Marekani ambayo ilipeleka manowari za kubebea ndege vita katika eneo la ukanda huo kuisaidia Israel inayoaminika kuwa na vikosi vyenye uwezo wa hali ya juu na  kuingia Ukanda wa Gaza imeambulia patupu kuwapata mateka wao wakiwemo wanajeshi jambo linaloibua maswali mengi.

Kitendo cha Jeshi la Israel cha kushindwa kuwapata na kuwakomboa mateka hao,kimeonesha kuwa Jeshi la Israel na washirika wake limeshindwa vita hivyo kwa kundi dogo lisilokuwa na vifaru,vifaa vya kisasa vya kijeshi zaidi ya kutumia silaha za kawaida katika kukabiliana na Jeshi la kisasa la Israel na washirika wake Marekani.

Mbali na hilo lakini pia Israel kukubali kusitisha vita kwa siku nne na kundi la Hamas ikiwemo  kubadilishana  wafungwa 150 wa kipalestina dhidi ya 50 wa Israel ni wazi kuwa MOSSAD haiwezi tena kukabiliana na kundi hilo hivyo Israel inapaswa kuwa makini kwa siku zijazo la sivyo itapigwa katika hatua za kushangaza hadi katika Mji Mkuu wake wa Jerusalem au Tel Aviv.

Israel pia imeshindwa kuliangamiza kundi hilo kama inavyoelezwa kutokana na kwamba licha ya Israel kufanya mashambulizi makali lakini viongozi wa Hamas wanaendelea na mikutano na viongozi wengi nje ya nchi,hivyo ni wazi kuwa haitaweszekana kuliangamiza kundi hilo ambalo nchi za Magharibi zinalitambua kama kundi la kigaidi lakini Urusi,Uturuki,Iran na baadhi ya nchi za kiarabu linawatambua kama wapigania uhuru wa Taifa la Palestina

Vita hivyo badala ya kuwaadhibu wanamgambo hao wa Hamas,vimewafanya wananchi wa Gaza-Palestina kutolewa kafara ambapo hadi sasa zaidi ya wapalestina 14,000 na zaidi ya 1000 raia wa Israel wameuawa

Next Post
Bajeti yaelemewa na vyeti vya pongezi kutoka Google

Bajeti yaelemewa na vyeti vya pongezi kutoka Google

COP 28,DUBAI

COP 28 Dubai-UAE

Tanzania yaanzisha Shahada ya Hali ya Hewa na Mabadiliko ya Tabianchi

Tanzania yaanzisha Shahada ya Hali ya Hewa na Mabadiliko ya Tabianchi

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In