• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Rais Vladimir Putin wa Urusi ‘si binadamu wa kawaida’

Apaa angani na dege la kijeshi linalobeba mabomu ya nyuklia

by bajeti
February 24, 2024
in Habari
0
Rais Vladimir Putin wa Urusi ‘si binadamu wa kawaida’

Rais wa Urusi Vladimir Putin (katikati) akiwa katika Kiwanda cha masuala ya Anga cha Kazan kilichopewa jina la Sergei Gorbunov,kinachotengenezandege za kimkakati za Tupolev zenye uwezo wa kubeba makombora ya nyuklia kilichopo, Jamhuri ya Tatarstan, Urusi(Picha na Sputnik)

Share on FacebookShare on Twitter

MOSCOW-Urusi

RAIS wa Urusi Vladimir Putin Alhamisi aliishangaza dunia baada ya kupaa angani akiwa kama rubani msaidizi wa ndege ya kijeshi ya  kubebea mabomu ya nyuklia.

Ndege hiyo ya kimkakati ya nyuklia aina ya TU-160M iliruka kutoka eneo la Kazan nchini humo kwa muda wa dakika 30 baada ya kufanyiwa maboresho makubwa ya kimkakati.

Rais Putin anaweza kuwa ndiye rais pekee duniani kutoka moja ya mataifa makubwa yenye kumiliki silaha za nyuklia kuruka na ndege za kijeshi akiwa kama rubani msaidizi bila kuogopa huku nchi yake ikiwa vitani na Ukraine.

Hata hivyo safari ya ndege ya Putin ya dakika 30  ​​pia ilionekana kutuma ujumbe kwa nchi za Magharibi wakiongozwa na Marekani kuwa nchi hiyo bado ina nguvu kubwa za kijeshi na haiogopi vikwazo ilivyowekewa wala haitaisitisha oparesheni zake za kijeshi.

Kuruka kwa ndege hiyo pia kunaashiria kuwa vita vya nchi hiyo na jirani yake Ukraine vinavyoingia mwaka wa tatu vinaweza kusababisha matumizi ya nyuklia ikiwa misaada wanayopewa Ukraine itafanikisha kuishinda Urusi

Putin, 71, ambaye jeshi lake limepata mafanikio makubwa katika vita vyake nchini Ukraine hivi karibuni baada ya kuliteka jiji la Adviika lililokuwa ngome kuu ya Jeshi la Ukraine.

Nchi za Magharibi ambazo zimetuma maelfu ya tani za makombora,mabomu,vifaru,risasi,magari na misaada mingine ili kulisaidia Jeshi la Ukraine kujilinda dhidi ya Urusi lakini misaada hiyo haijasaidia katika kulifanya Jeshi la Ukraine kurudisha maeneo yaliyotekwa na Urusi.

Siku ya Alhamisi, vyombo vya habari vya Urusi vilimuonesha Rais Putin, akiwa amevalia mavazi ya rubani, alipanda ndege ya kivita katika uwanja wa ndege uliofunikwa na theluji wa kiwanda cha kutengeneza ndege katika mji wa Mto Volga wa Kazan.

Kiwanda hicho kilipokea maagizo ya serikali kutoa toleo la kisasa la  Tu-160 ambalo liliruka kwa mara ya kwanza miaka ya 1980 na lilipewa jina la Blackjack na NATO.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya safari ya kuruka,Rais Putin aliisifu ndege hiyo mpya kama “bora,” akibainisha kuwa ina maboresho makubwa ikilinganishwa na toleo la awali.

Safari ya ndege ya Alhamisi ilikuwa angalau mara ya tatu alipoingia kwenye chumba cha marubani cha ndege za kivita.

Mnamo 2000,Rais Putin alichukua kiti cha rubani msaidizi katika ndege ya kijeshi aina ya  Su-27 na kuruka hadi Chechnya wakati wa mapigano ya kujitenga na mnamo 2005 aliongoza ndege ya Tu-160 wakati wa mazoezi ya kijeshi. lakini pia Rais Putin alikuwa rubani msaidizi katika ndege ya amphibious,

Rais Putin ambaye hazungumzi mara kwa mara zaidi ya kuonesha vitendo,aliwahi pia kuonekana akiendesha gari juu ya daraja kubwa linalounganisha Rasi ya Crimea na nchi hiyo baada ya kufanyiwa maboresha miezi kadhaa tangu liliposhambuliwa na vikosi vya Ukraine

Katika hatua nyingine,Rais huyo wa Urusi hajawahi kuonekana akiwa na mkewe katika hala zote wala safari za nje ya nchi yake  tofauti na marais wengine duniani.

Next Post
Kanisa Katoliki laanza mchakato wa kumtangaza Hayati Mwalimu Julius Nyerere kuwa Mtakatifu

Kanisa Katoliki laanza mchakato wa kumtangaza Hayati Mwalimu Julius Nyerere kuwa Mtakatifu

CCM-Zanzibar:Wananchi wanahitaji siasa za kuvumiliana na ustaarabu

CCM-Zanzibar:Wananchi wanahitaji siasa za kuvumiliana na ustaarabu

Jeshi la Polisi Songwe na mikakati ya ulinzi na usalama

Jeshi la Polisi Songwe na mikakati ya ulinzi na usalama

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In