NA MWANDISHI WETU
bajetinews@gmail.com
KANISA Katoliki nchini Tanzania limeanza mchakato wa kumtangaza Mtakatifu Baba wa Taifa hilo Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyefariki dunia mnamo Oktoba 14,2019 nchini Uingereza.
Nyerere ambaye ndiye Rais wa kwanza wa Taifa hilo lenye historia ya ukarimu na amani,alitawala tangu Desemba 9, 1961 baada ya kupata uhuru wake kutoka kwa waingereza na kisha kuachia madaraka kwa hiyari.
Hata hivyo Nyerere ndiye mwasisi wa ukombozi wa mataifa mengi ya Kusini mwa Afrika.
Uamuzi wa Kanisa hilo umekuja wakati ambapo taarifa kutoka nchini Uganda zikieleza kuwa tayari mchakato huo ulishaanza miaka kadhaa nyuma juu ya kutangazwa kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuwa mwenye Heri na Mtakafu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Februari 25,2024 na Kanisa hilo Jimbo Kuu la Dar es Salaam na kusainiwa na Askofu Mkuu Juda Thadaeus Ruwa’ichi ameeleza kuwa ameunda Mahakama ya Jimbo Kuu la Dar es Salaam inayoshughulikia mchakato wa kutangazwa Mwenye Heri na Mtakatifu ,Mtumishi wa Mungu Julius Kambarage Nyerere.
Ameeleza kuwa Mahakama hiyo ya kijimbo itashughulikia ufuatiliaji wa maisha ,fadhila kubwa na sifa za utakatifu na nguvu ya maombezi ya Mtumishi wa Mungu.
”Mhashamu Askofu Mkuu JudeThadeus Ruwaichi ameunda Mahakama hiyo baada ya ombi lililowasilishwa kwake Julai 23,2023 na Bruda Reginald D.Cruz wa Shirika la Wamisionari wa Afrika ,aliyeteuliwa kisheria kuwa Mratibu wa Mchakato huo na Mshashamu Askofu Mkuu Gervas John Nyaisonga ,Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania na mwombaji wa kufanyika kwa mchakato huo.
”Hivyo Askofu Mkuu Ruwaichi anamualika yeyote mwenye taarifa yoyote ,iwe ya kufaa au isiyofaa kuhusu maisha na fadhila kubwa sana za Mtumishi wa Mungu kama Mwamini Mlei Mkatoliki na Baba wa familia.
”Pia taarifa kuhusu sifa zake za Utakatifu na nguvu ya maombezi yake,kuziwasilisha kwenye Mahakama hiyo ya Jimbo Kuu la Dar es Salaam inayoshughulikia mchakato huo’’amesema Ruwaichi”amesema Askofu Ruwa’ichi
Askofu Ruwaichi amebainisha kuwa kwa kuwa kuna taratibu za ushahidi wa kisheria ,maandiko yote yanayodhaniwa kuwa yake yanapaswa kukusanywa.
”Kwa tangazo hilo inaelekezwa kwamba yeyote ambaye ana maandiko hayo ,pamoja na nyaraka zozote zilizoandikwa na Mtumishi wa Mungu ambazo bado hazijakabidhiwa kwa Mratibu wa Mchakato ayatume kwa umakini kwa Mahakama hiyo.
”Inakumbushwa kwamba neno ‘’maandiko’’isielewe kama machapisho tu ambayo yameshakusanywa bali pia miswada,shajara,barua na maandishi binafsi ambavyo vinaweza kudhihirisha maisha ya kiroho ya Mtumishi wa Mungu Julius Kambarage Nyerere na wale wanaohitaji kubaki na maandiko halisi wanaweza kuwasilisha nakala iliyothibitishwa ipasavyo”ameongeza Askofu Ruwa’ichi
Hata hivyo tangazo hilo litabaki kwa muda wa miezi sita katika milango yote ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu na makanisa yote ya maparokia ya Metropolitani ya Dar es salaam




Discussion about this post