• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Siasa

CCM-Zanzibar:Wananchi wanahitaji siasa za kuvumiliana na ustaarabu

Wanachama na viongozi waombwa kujibu hoja kwa hoja

by bajeti
March 11, 2024
in Siasa
0
CCM-Zanzibar:Wananchi wanahitaji siasa za kuvumiliana na ustaarabu

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,akizungumza na Wanachama wa CCM Zanzibar.

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,ZANZIBAR

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar,kimesema wananchi wanahitaji siasa za   kuvumiliana na ustaarabu ikiwemo wanavyonufaika kiuchumi na kijamii huku nchi ikipiga hatua kubwa za maendeleo.

Hata hivyo wanachama na viongozi wa chama hicho wametakiwa kujibu hoja kwa hoja huku wakitangaza na kuhamasisha kwa kasi kubwa mambo yaliyotekelezwa na Serikali mijini na vijijini kwa maslahi ya wananchi.

Kauli hiyo imetolewa na Machi 11,2024 na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,wakati akizungumza na wanachama na viongozi wa Chama hicho huko Jimbo la Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja Visiwani Zanzibar.

Dkt.Dimwa amesema vyama vya siasa Zanzibar vimepoteza muelekeo na mvuto kwa wananchi kutokana na kasi kubwa ya utekelezaji wa Ilani ya chama hicho ya mwaka 2020-2025.

Ameongeza kuwa kuna baadhi ya wanasiasa wanatumia vibaya uhuru wa kutoa maoni na badala yake wanatoa kauli za kumdhalilisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ally Mwinyi huku wakipandikiza kauli za uchochezi kwa wananchi.

Hata hivyo Dkt.Dimwa,amevitaka Vyombo vya Ulinzi na Usalama kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua za kisheria wanasiasa hao na watu wengine wanaovunja sheria kwa makusudi kwa kumdhalilisha Rais wa Zanzibar ikiwemo kuthibiti  upotoshaji unaondikwa katika mitandao ya kijamii nchini kwa lengo la kumdhalilisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Aidha amebainisha kuwa CCM itaendelea kulinda kwa vitendo heshima,hadhi thamani ya Rais wa Zanzibar na wasaidizi wake kwani wapo katika mamlaka yanayotokana na Chama Tawala cha CCM kupitia ridhaa halali ya uchaguzi wa Kidemokrasia chini ya matakwa ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.

“Juzi Chama Cha ACT-Wazalendo wamefanya mapokezi ya Viongozi wao lakini jambo la kusikitisha mikutano yao kwa Unguja na Pemba imepambwa na kauli chafu dhidi ya  Rais wetu mpendwa Dk.Hussein Mwinyi,hatuwezi kuvumilia utovu huo wa nidhamu kwani haukubaliki kisiasa,kidini na kitamaduni.

”Tabia hizo zinafanya tuanze kutilia mashaka kama kweli wenzetu wana nia ya dhati ya kuendelea na Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) au wana ajenda zao binafsi kuirejesha Zanzibar katika machafuko ya kisiasa”,amesema  Dkt.Dimwa.

Next Post
Jeshi la Polisi Songwe na mikakati ya ulinzi na usalama

Jeshi la Polisi Songwe na mikakati ya ulinzi na usalama

Donge -Zanzibar

Donge -Zanzibar

Uwanja wa ndege Abeid Aman Karume watangazwa kuwa bora zaidi barani Afrika.

Uwanja wa ndege Abeid Aman Karume watangazwa kuwa bora zaidi barani Afrika.

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 13,062
  • Total page views 14,807

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In