• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Uwanja wa ndege Abeid Aman Karume watangazwa kuwa bora zaidi barani Afrika.

by bajeti
March 16, 2024
in Habari
0
Uwanja wa ndege Abeid Aman Karume watangazwa kuwa bora zaidi barani Afrika.

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Aman Abeid Karume uliopo Zanzibar

Share on FacebookShare on Twitter

 

NA MWANDISHI WETU ZANZIBAR

UWANJA  wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume wa visiwani Zanzibar  umetangazwa kuwa moja ya viwanja bora zaidi vya ndege barani Afrika.

Hayo yameelezezwa Machi 15,2024 na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar, Seif Abdallah Juma  baada ya uwanja huo kutunukiwa tuzo za Ubora wa Huduma za Viwanja vya Ndege zinazotolewa na Baraza la Viwanja vya Ndege Kimataifa ambayo ni taasisi inayojihusisha na huduma za viwanja vya ndege kwa lengo la kuunganisha utendaji wa sekta hiyo kwa viwango vya kimataifa

Amesema tuzo hizo za Ubora wa Huduma za Viwanja vya Ndege zinazotolewa na Baraza la Viwanja vya Ndege Kimataifa hutolewa kila mwaka na zinazingatia ubora wa uwanja wa ndege kulingana na maoni ya abiria yaliyokusanywa kupitia tafiti za kila siku katika maeneo ya kuondoka na kuwasili abiria hao kote duniani

”Tuzo hizo zinazingatia ubora wa uwanja wa ndege kulingana na maoni ya abiria yaliyokusanywa kupitia tafiti za kila siku katika maeneo ya kuondoka na kuwasili abiria hao kote ulimwenguni na hii itaongeza idadi ya watalii wanaotembelea visiwa vya Zanzibar”amesema  Juma

Aidha ameongeza kuwa tuzo hizo zinatolewa kwa kuzingatia vielelezo mbalimbali ikiwa ni pamoja na wafanyakazi waliojitolea zaidi, wepesi zaidi wa safari kwenye uwanja wa ndege, uwanja wa ndege wenye mvuto zaidi na uwanja wa ndege msafi zaidi.

” Mafanikio haya yametokana na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) katika kuvutia uwekezaji mkubwa kwenye sekta hiyo”amesema Juma

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume ndio uwanja wa ndege pekee wa kimataifa visiwani Zanzibar ambapo watalii wengi huwasili visiwani Zanzibar humo kila mwaka kutokana na vivutio vyake vya kila aina yakiwemo maeneo ya kale na fukwe za kuvutia

Next Post
Dawa ya kuwatambua ‘wachawi ’yaua watu 50

Dawa ya kuwatambua ‘wachawi ’yaua watu 50

Serikali kuwashirikisha wananchi matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022

Serikali kuwashirikisha wananchi matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022

CCM-Zanzibar:ACT-Wazaleno haina hati miliki ya Zanzibar

CCM-Zanzibar:ACT-Wazaleno haina hati miliki ya Zanzibar

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:5
  • Today's page views 5
  • Total visitors 13,061
  • Total page views 14,806

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In