• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Serikali kuwashirikisha wananchi matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022

by bajeti
March 16, 2024
in Habari
0
Serikali kuwashirikisha wananchi matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022

Spika wa Bunge Mstaafu ambaye ni Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO

SERIKALI ya Tanzania imo katika hatua ya mwisho ya kuwashirikisha wananchi matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 ili waweze kupanga mipango yao ya kimaendeleo ikiwemo kiuchumi kijamii na kisiasa katika maeneo yao kuanzia ngazi ya Kata,Kijiji na Kitongoji

Hayo yameelezwa mkoani Dar es Salaam na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 Anne Makinda wakati wa Mafunzo kwa  Wanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Dar es Salaa (DCPC) kuhusu Usambazaji na Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 yaliyoandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) yaliyofanyika Machi 13 na 14,2024.

Amesema Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 ni tofauti na Sensa za miaka iliyopita ambapo baada ya kufanyika hakuna tena muendelezo wake kwa wananchi lakini safari hii Rais Samia Suluhu Hassan alizindua Mwongozo wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 ambapo sasa  matokeo hayo yanawafikia wananchi  kuanzia ngazi za chini kwa uwazi.

Amesema hiyo ni Sensa ya sita kufanyika nchini ambapo  awamu ya kwanza ilikuwa ni kutangazwa na kuhamasisha na awamu ya pili ni kufanyika kwa Sensa hiyo ambapo sasa ni awamu ya tatu kwa wananchi  kupata matokeo hayo ili kupanga mipango ya maendeleo na serikali katika maeneo yao.

‘’Kila mwananchi anauwezo wa kujua taarifa katika Kijiji chake na wanasiasa shangilie lakini Sensa ni kiboko kwa kuwa kwenye takwimu hakuna makandokando  kwani Sensa hii inaonesha kila kitu kuanzia ngazi ya chini hivyo wananchi wanapojua matokeo ya Sensa katika eneo lao itasadia kuzungumza wanachodai’’amesema Makinda

Aidha amebainisha  kuwa sekta  ya habari ni daraja muhimu kati ya wananchi na Serikali na ina mchango wa kipekee katika kuleta maendeleo ya kiuchumi,kisiasa,kijamii ambapo ilifanya kazi kubwa wakati wa  kuanza kwa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022.

‘’Mafanikio ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 ni mfano bora wa kazi iliyofanywa na vyombo vya habari na sisi tunawafundisha Wakuu wa Mikoa,Madiwani,Makatibu  Wakuu,Wakuu wa Wilaya juu ya matokeo hayo kwani humo kuna matokeo mengi sana hivyo hata waandishi wa habari itawasaidia zaidi katika kufanya kazi zenu’’ameongeza Makinda

Akizungumza kwa niaba ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Dkt.Albina Chuwa,Meneja wa Takwimu na Mratibu wa Sensa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Kapala amesema waandishi wa habari ni watu muhimu katika zoezi hilo kwa kuwa wanasaidia kufikisha taarifa  za sensa kwa watu wa hali ya chini

Naye Mwenyekiti wa DCPC Samson Kamalamo ameishukuru Serikali kwa kuandaa mafunzo hayo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Dar es Salaam ili kuwa sehemu ya mapango wa utekelezaji wa awamu ya tatu ya kuwafikisha wananchi matokeo hayo ya Sensa ya Mwaka 2022.

‘’Naishukuru sana Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kuishirikisha DCPC  kwa kuwa inagusa asilimia 75 ya vyombo vyote vya habari Tanzania na tunafurahi kuona vyombo vya habari ni muhimu katika utekelezaji wa awamu hii ya tatu ya usambazaji na matumizi ya matokeo hayo wananchi’’amesema Kamalamo   

Next Post
CCM-Zanzibar:ACT-Wazaleno haina hati miliki ya Zanzibar

CCM-Zanzibar:ACT-Wazaleno haina hati miliki ya Zanzibar

ZAMBIA

ZAMBIA

Mwanga-Tanzania

Mazungumzo

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 13,062
  • Total page views 14,807

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In