• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Urusi yatangaza rasmi kuwa iko vitani na Ukraine

Raia wake 40 wauawa na wengine zaidi ya 100 wajeruhiwa katika shambulizi ya kigaidi Moscow

by bajeti
March 22, 2024
in Habari
0
Urusi yaichanganya dunia,EU yasema sasa ni hatari zaidi kuliko awali

Rais wa Urusi Vladmir Putin

Share on FacebookShare on Twitter

 

MOSCOW,URUSI

URUSI imetangaza rasmi kuwa ipo vitani na Ukraine huku watu 40 wakiuawa na zaidi ya 100 kujeruhiwa katika “shambulio lililotokea katika jumba la maduka la Crocus City Hall na eneo la tamasha, kaskazini magharibi mwa Moscow,

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Urusi vilieleza kuwa Huduma ya Usalama ya Shirikisho la Urusi (FSB) iliripoti Ijumaa kuwa shambulizi hilo ni la kigaidi na limefanywa na kundi la watu wenye silaha waliovamia katika Ukumbi wa Jiji la Crocus nje ya Moscow siku ya Ijumaa usiku.

Kulingana na video zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii, zimeonesha jinsi watu liokuwa katika ukumbi wa sinema wakikimbia hovyo huku maeneo mengine yakiwaka  moto baada ya watu hao kuanza kuwafyatulia risasi wageni kiholela.

Haijabainika iwapo magaidi hao bado wako kwenye jengo hilo ambapo shughuli ya kuwahamisha wageni na majaribio ya kuzima moto huo yanaendelea.

Duka hilo liko katika mji wa Krasnogorsk, kaskazini magharibi mwa Moscow na lina maduka mengi ya hali ya juu na ukumbi mkubwa wa muziki.

Kulingana na Wizara ya Hali za Dharura, takriban watu 100 wamesindikizwa hadi mahali salama na wazima moto na inakadairiwa kuwa watu 6,200 walikuwa kwenye jengo hilo wakati wahambuliaji walipofyatuaji risasi.

Washambuliaji walishambulia kabla ya tamasha la bendi ya muziki wa rock “Picnic Kabla ya tukio hilo

Awali Msemaji wa Ikulu ya Urusi, Kremlin Dmitry Peskov amesema ,operesheni ya kijeshi ya Urusi nchini Ukraine imegeuka kuwa vita kamili baada ya nchi za Magharibi kuwa mshiriki katika mzozo huo,

Amesema Moscow itaendelea kutekeleza lengo lake la kuhakikisha kuwa jeshi la Ukraine haliwezi kuwa tishio kwa raia au eneo la Urusi,  Peskov ameliambia gazeti la Argumenti i Fakty, kuwa nchi hiyo sasa ina masomo manne mapya ya shirikisho ambayo lazima yalindwe na kukombolewa kikamilifu kutoka vikosi vya Kiev

 

Next Post
Mkutano SADC

Mkutano SADC

Balozi Dkt Nchimbi: Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar(SUK) imeondoa siasa za chuki na uhasama

Balozi Dkt Nchimbi: Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar(SUK) imeondoa siasa za chuki na uhasama

Mumbai:Jiji la tatu duniani kukaliwa na  mabilionea wengi

Mumbai:Jiji la tatu duniani kukaliwa na mabilionea wengi

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In