• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Mumbai:Jiji la tatu duniani kukaliwa na mabilionea wengi

Yalishinda Jiji la Beijing nchini China

by bajeti
March 26, 2024
in Habari
0
Mumbai:Jiji la tatu duniani kukaliwa na  mabilionea wengi

Jiji la Mumbai nchini India

Share on FacebookShare on Twitter

NEW DELH,INDIA

JIJI la Mumbai nchini India limetajwa kuwa ndio jiji linalokaliwa na mabilionea wengi katika Bara la Asia  na kushika nafasi ya tatu duniani baada ya New York la Marekani na London nchini Uingereza.

Mumbai umeipiku Jiji la Beijing  nchini China na kuwa ‘mji mkuu wa mabilionea’ wa Asia kwa mara ya kwanza.

Kulingana na Taasisi ya Utafiti ya Hurun yenye makao yake makuu Shanghai nchini China,imeeleza kuwa  idadi ya mabilionea katika kitovu cha kifedha cha India ilipanda hadi 92, na kushika namba tatu  juu zaidi ulimwenguni baada ya New York inayokaliwa na mabilionea 119 na London 97.

Hata hivyo, Mji Mkuu wa India New Delhi umeingia kwenye 10 bora kwa mara ya kwanza.

Kulingana na taasisi hiyo India ina mabilionea 271, ambayo ni ya tatu kwa juu zaidi duniani, nyuma ya China 814 na Marekani 800.

Mmiliki wa Kampuni ya India Reliance Industries Mukesh Ambani , amebaki na nafasi yake kama Mhindi tajiri zaidi na ana utajiri wa dola za kimarekani Bilioni 115, ambayo pia inamfanya kuwa mtu tajiri zaidi barani Asia.

Tajiri wa pili kwenye orodha hiyo ni Mwenyekiti wa  Adani Gautam Adani mwenye utajiri wa (dola za kimarekani bilioni 86), ambaye utajiri wake umeongezeka kwa asilimia 33.

Mwenyekiti na Mtafiti Mkuu wa Ripoti ya  Hurun Rupert Hoogewerf amesema  akili ya bandia (AI) imekuwa kichocheo kikuu cha mwenendo huo, ikizalisha zaidi ya nusu ya utajiri wote mpya mwaka huu.

Idadi ya mabilionea nchini India imeongezeka kwa kasi tangu nchi hiyo ilipofanyia mageuzi sera yake ya kiuchumi mwaka 1991 ili kuruhusu uwekezaji zaidi wa kigeni.

Hata hivyo, tofauti ya utajiri kati ya asilimiamoja  ya juu na maeneo mengine ya nchi imefikia viwango vya juu vya kihistoria.

Next Post
Wenye ulemavu wa miguu sasa kuendesha magari

Utafiti:Asilimia tatu ya kaya za Tanzania ndizo zinazomiliki magari

Ulinzi na Usalama kwa wanafunzi

Ulinzi na Usalama kwa wanafunzi

Uchumi wa Tanzania kukua kwa asilimia sita

Uchumi wa Tanzania kukua kwa asilimia sita

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:8
  • Today's page views 8
  • Total visitors 13,064
  • Total page views 14,809

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In