• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

TMDA:Waandishi andikeni habari za Dawa, Vifaa Tiba na Bidhaa za Tumbaku zenye kuleta tija kwa jamii

by bajeti
May 17, 2024
in Habari
0
TMDA:Waandishi andikeni habari za Dawa, Vifaa Tiba na Bidhaa za Tumbaku zenye kuleta tija kwa jamii

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA) Dkt.Adm Fimbo (kushoto) akiwa na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari walioshinda tuzo za uandishi bora wa habari za Dawa,Vifaa Tiba na Bidhaa za Tumbaku zilizoandaliwa na mamlaka hiyo Mei 16,2024 mkoani Iringa.(Picha na mpigapicha wetu)

Share on FacebookShare on Twitter

MWANDISHI WETU,IRINGA.

MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA),imewataka waandishi wa habari nchini kuendelea kuandika habari za dawa, vifaa tiba na bidhaa za tumbaku zenye kuleta tija kwa jamii.

Aidha TMDA inatambua kazi kubwa inayofanywa na waandishi wa habari katika kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya Dawa na vifaa tiba  ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza endapo dawa hizo hazitatumiwa ipasavyo.

Wito huo umetolewa Mei 17,2024 mkoani Iringa na Mkurugenzi Mkuu wa TMDA Dkt. Adam Fimbo wakati wa utoaji wa tuzo kwa waandishi wa habari bora wa Uandishi wa Habari za Dawa, Vifaa Tiba, Vitendanishi na Bidhaa za Tumbaku kwa mwaka 2024 .

Amesema TMDA inatambua mchango wa waandishi wa habari hivyo kuifanya Mamlaka hiyo kuandaa tuzo kwa wanahabari watanaondika habari za TMDA zenye kuleta tija kwa jamii

Ameongeza kuwa tuzo hizo ni sehemu ya jitihada za TMDA wanazozifanya kwa waandishi wa habari katika kuripoti habari za dawa, vifaa tiba, bidhaa za tumbaku na vitendanishi katika kuuhabarisha umma wa watanzania.

“Tunataka mtuandike mambo yote ambayo mmeyachunguza vizuri yaandikwe ili tujirekebishe.

“Tuzo hizi ni maazimio ya kikao kazi yaliyofanyika mkoani Arusha Mwaka 2021 ambapo Mwaka 2022  tulianza utekelezaji wake,”amesema Dkt.Fimbo

Hata hivyo Dkt.Fimbo amewahimiza waandishi wa habari kuendelea kuelimisha jamii bila kuchoka kwani wana nafasi kubwa ya kuwafikia Wananchi.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA) Dkt.Adam Fimbo akimkabidhi tuzo ya uandishi bora wa habari za Dawa,Vifaa Tiba na Bidhaa za Tumbaku mwandishi wa habari kutoka blogu Matukio Daima Andrew Chale Mei16,2024 mkoani Iringa(Picha na mpigapicha wetu)

Waandishi walioshinda tuzo hizo ni Veronica Mrema kutoka blogu ya Matukio na Maisha, ,Madina Mohammed  wa blogu ya Wamachinga TV, Penina Malundo kutoka Times Majira na mshindi wa nne akiwa ni Andrew Chale   wa Matukio Daima

Utoaji wa tuzo hizo pia uliambatana na kikao kazi cha wahariri na waandishi wa habari juu ya utekelezaji wa Sheria ya  Dawa na Vifaa Tiba, Sura 219.

Next Post
Tunapanda miti

Tunapanda miti

DC Nassari awataka vijana kusoma kwa bidii kufikia malengo yao

DC Nassari awataka vijana kusoma kwa bidii kufikia malengo yao

Korea Kaskazini,Kusini zatumiana takataka kupitia maputo

Korea Kaskazini,Kusini zatumiana takataka kupitia maputo

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In