• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Michezo

DC Nassari awataka vijana kusoma kwa bidii kufikia malengo yao

by bajeti
May 31, 2024
in Michezo
0
DC Nassari awataka vijana kusoma kwa bidii kufikia malengo yao
Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,MAGU

MKUU wa Wilaya ya Magu mkoani Mwanza Joshua Nassari amewataka vijana wilayani humo kuongeza juhudi katika masomo ili waweze kufikia malengo yao na kuinua kiwango cha taaluma katika eneo hilo.

Nassari ametoa kauli hiyo wilayani humo wakati akipokea vikombe vya ushindi baada ya Halmashauri ya Wilaya ya Magu kushika nafasi ya kwanza kimkoa katika Mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA).

Magu ambayo imefanya vizuri katika mshaindano hayo kwa kuchukua  vikombe 13 katika fani za Mpira wa Kikapu Wavulana na Wasichana, Riadha , Kwaya, Ngoma, Mpira wa miguu wavulana, Handball , Usafi na Nidhamu pamoja na Kombe la Mshindi wa Jumla katika Halmashauri zote za Mkoa wa Mwanza zilizoshiriki mashindano hayo.

Akizungumza wakati akipokea vikombe hivyo  Mei 31,2024,Nassari  amewapongeza vijana  hao kwa kufanya  vizuri katika mashindano hayo nakuwaomba  kuongeza bidii na kufanya vizuri zaidi katika mashindano  ya Kitaifa.

Amesema ni muhimu sana kwa  wanafunzi hao kutumia ushindi huo katika kuongeza juhudi na bidii katika taaluma na kufanya vizuri katika masomo yao ili kufikia malengo yao na kuifanya wilaya ifanye vizuri katika taaluma.

Naye  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu Mohamed Ramadhani ametoa pongezi kwa wote waliofanikisha ushindi na kuwataka wafanye vizuri zaidi kwa mashindano mengine mwaka 2025.

Awali akitangaza matokeo hayo,Afisa Utamaduni wa Wilaya ya Magu, Peter Mujaya amesema Magu imebeba vikombe 13 katika fani ya Mpira wa Kikapu Wavulana na Wasichana nafasi ya kwanza, Mpira wa mikono wavulana nafasi ya pili, na wasichana nafasi ya tatu, Riadha wasichana nafasi ya kwanza na wavulana nafasi ya tatu.

Kwa upande wa nafasi ya  Kwaya,Mujaya amebainisha kuwa wameshika  nafasi ya kwanza, Ngoma nafasi ya pili , Muziki nafasi ya tatu, Mpira wa miguu nafasi ya tatu, Usafi na Nidhamu nafasi ya kwanza, Mpira wa wavu nafasi ya tatu  pamoja na Kombe la Mshindi wa Jumla kwa Mkoa wa mwanza.

Vijana 26 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Magu wameteuliwa kuunda timu ya mkoa itakayoshiriki mashindano ya UMITASHUMTA Taifa yatakayofanyika mwezi  Juni  mkoani Tabora.

Next Post
Korea Kaskazini,Kusini zatumiana takataka kupitia maputo

Korea Kaskazini,Kusini zatumiana takataka kupitia maputo

Mke,’mchepuko’ kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya mumewe

Mke,'mchepuko' kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya mumewe

Dkt.Chana:Maliasili  yatengewa bajeti zaidi ya Sh.Bilioni 600

Watoto zaidi ya Milioni 200 wanatumikishwa duniani,Kilimo chaongoza

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 13,062
  • Total page views 14,807

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In