• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Korea Kaskazini,Kusini zatumiana takataka kupitia maputo

by bajeti
June 4, 2024
in Mazingira
0
Korea Kaskazini,Kusini zatumiana takataka kupitia maputo

Puto

Share on FacebookShare on Twitter

SEOUL,KOREA KUSINI

WAKATI mizozo ikiongozeka duniani kutokana na uwepo wa ushindani wa pande mbili za wale wanaoziunga mkono Marekani na washirika wake wa nchi za Magharibi na  wanaoziunga mkono Urusi na washirika wake ikiwemo China,Korea Kaskazini na Kusini zimekuwa zikitumiana takataka kupitia maputo yanayorushwa angani.

Korea Kaskazini ambayo inaungwa mkono na China,Urusi na Iran inadaiwa kuwa imekuwa ikituma maputo ya takakata kuelekea Korea Kusini inayoungwa mkono na Marekani na nchi za Magharibi ambayo nayo imekuwa ikituma  maelfu ya vipeperushi vinavyoipinga Serikali ya Korea Kaskazini.

Kwa mujibu wa taarifa ya tovuti ya Kituo cha habari cha Serikali ya  Japan ya NHK kimeeleza kuwa Korea Kaskazini  itasitisha kwa muda kutuma maputo yaliyojazwa takataka nchini Korea Kusini na kuonya kuwa  inaweza kuendelea na operesheni hiyo ikiwa upande wa Korea Kusini utatuma vipeperushi zaidi vya kupinga Korea Kaskazini nchini Korea Kaskazini.

NHK imetangaza kuwa Korea Kaskazini imekuwa ikituma maputo yaliyojazwa taka tangu wiki iliyopita kwa kile kilichoelezwa kulipiza kisasi dhidi ya vitendo vya baadhi ya wanaharakati nchini Korea Kusini ambao  walituma maputo yenye vipeperushi vya kukosoa uongozi wa Korea Kaskazini nchini Korea Kaskazini.

Ofisi ya Rais wa Korea Kusini ilikuwa imetoa onyo siku ya Jumapili kwamba itachukua hatua “zisizovumilika” dhidi ya Korea Kaskazini, ikiwa haitaacha kutuma maputo yaliyojazwa taka.

Muda mfupi baada ya onyo hilo la Korea Kusini,Makamu wa Waziri wa Ulinzi wa Korea Kaskazini Kim Kang Il alitangaza kwamba operesheni ya puto ilikuwa inasitishwa kwa muda na kuongeza kuwa Korea Kaskazini ilituma tani 15 za taka za karatasi.

Next Post
Mke,’mchepuko’ kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya mumewe

Mke,'mchepuko' kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya mumewe

Dkt.Chana:Maliasili  yatengewa bajeti zaidi ya Sh.Bilioni 600

Watoto zaidi ya Milioni 200 wanatumikishwa duniani,Kilimo chaongoza

Marafiki wa Serengeti Uswisi watoa vifaa vya zaidi ya Sh.Milioni 40 kwa TAWA kulinda rasilimali za wanyamapori

Marafiki wa Serengeti Uswisi watoa vifaa vya zaidi ya Sh.Milioni 40 kwa TAWA kulinda rasilimali za wanyamapori

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In