• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Watoto zaidi ya Milioni 200 wanatumikishwa duniani,Kilimo chaongoza

by bajeti
June 6, 2024
in Habari
0
Dkt.Chana:Maliasili  yatengewa bajeti zaidi ya Sh.Bilioni 600

Waziri wa Katiba na Sheria Balozi Dkt Pindi Chana

Share on FacebookShare on Twitter

NA ANDREW CHALE

WATOTO zaidi ya Milioni 200 wanatumikishwa katika kazi mbalimbali duniani huku  Milioni 73 kati yao wakiwa chini ya umri wa miaka 10.

Hata hivyo Sekta ya Kilimo imetajwa kuongoza kwa kuajiri watoto wengi hasa katika mashamba ya chai, tumbaku, miwa, mwani, karafuu na shughuli za uvuvi.

Taarifa hiyo imetolewa wakati wa kongamano la kujadili ulinzi wa mtoto  kuwa kamati  lililoandaliwa na Mtandao wa Kupinga Utumikishwaji wa Watoto na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Juni 5,2024 jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo Kongamano hilo limekuja wakati Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria wa Mwaka 2022 (DHS-MIS 2022) uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania (NBS) kueleza kuwa kaya za Tanzania zina wastani wa watu 4.5 huku  asilimia 29 ya kaya hizo zikiongozwa na wanawake.

Utafiti huo umebainisha kuwa  takribani nusu (sawa na asilimia 46) ya watu wote katika kaya hizo za Tanzania ni watoto wa umri chini ya miaka 15.

Kutokana na utafiti huo,Kongamano hilo linaweza kusaidia katika kuhakikisha watoto wanalindwa dhidi ya utumikishwaji na vitendo vya ukatili dhidi yao yakiwemo mauaji.

Akizungumza katika kongamano hilo, Waziri wa Katiba na Sheria,Balozi Dkt. Pindi Chana  amesema Serikali inakwenda kuweka sheria kali zitakazomlinda mtoto hapa nchini ambapo jopo la mawaziri wa wizara zaidi ya nne watakutana kwenye Kamati Maalum.

Balozi Dkt. Chana amebainisha kuwa  jopo hilo litaundwa na Kamati  ya Wizara ya Mambo ya Ndani, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Maendeleo ya Jamii na Wizara ya Katiba na Sheria  ili kuangalia chanzo ni nini kinachosababisha ukatili kwa watoto nchini.

Aidha ameongeza  kuwa jopo hilo litaangalia chanzo cha ukatili huo na kisha wataweka mikakati ili kudhibiti unyanyasaji huo.

“Tumekubaliana tukutane tuweke mikakati ya kuangalia vyanzo vya ukatili kwa watoto, tutashirikiana na familia, shule, taasisi za dini ili tuweze kudhibiti ukatili.

‘’Umefika wakati wa kuweka mikakati ili kuhakikisha mtoto anapata haki zake ikiwemo ya elimu, matibabu na kulindwa dhidi ya utumikishwaji na shughuli nyingine’’amesema Balozi Dkt.Chana

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UN Global Compact Chapa ya Tanzania, Marsha Yambi, amesema watoto Milioni 200 wanatumikishwa katika kazi mbalimbali duniani ambapo kati yao Milioni 73 wako chini ya miaka 10.

Yambi amebainisha kuwa Sekta ya  Kilimo ndio inaongoza kwa kuajiri watoto wengi hasa katika mashamba ya chai, tumbaku, miwa, mwani, karafuu na shughuli za uvuvi.

“Sekta binafsi inaonekana inachangia kuajiri watoto wadogo kwenye mashamba, tuhakikishe watoto hawawi katika ajira na tupate faida kwa haki na siyo kwa kupitia watoto,” amesema Yambi.

Mratibu wa Mtandao wa Kupinga Utumikishwaji wa Watoto nchini, Scholastica Pembe, amesema kongamano hilo limelenga kujadili sera na sheria zinazomlinda mtoto na ikiwemo  Sheria ya Ndoa ambayo inaruhusu mtoto aolewe chini ya miaka 18.

Pembe ameitaja Sheria ya Kazi  ambayo pia inaruhusu mtoto aanze kufanya kazi kuanzia miaka 14 na kuendelea lakini afanyishwe kazi ambazo si hatarishi na apate muda wa kucheza.

Next Post
Marafiki wa Serengeti Uswisi watoa vifaa vya zaidi ya Sh.Milioni 40 kwa TAWA kulinda rasilimali za wanyamapori

Marafiki wa Serengeti Uswisi watoa vifaa vya zaidi ya Sh.Milioni 40 kwa TAWA kulinda rasilimali za wanyamapori

TANROADS:Ujenzi wa BRT hautaathiri sanamu la askari  lililopo Posta-Dar es salaam

TANROADS:Ujenzi wa BRT hautaathiri sanamu la askari lililopo Posta-Dar es salaam

TAWA:Tumedhibiti utoroshwaji wa Nyara za Serikali katika Uwanja wa Ndege JNIA

TAWA:Tumedhibiti utoroshwaji wa Nyara za Serikali katika Uwanja wa Ndege JNIA

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In