• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Wanawake zaidi ya 800 wakamatwa wakijihushisha na biashara ya dawa za kulevya

by bajeti
July 14, 2024
in Habari
0
Wanawake zaidi ya 800 wakamatwa wakijihushisha na biashara ya dawa za kulevya

Taarifa ya Dawa za Kulevya kwa mwaka 2023 iliyotolewa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (CDEA)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

WANAWAKE zaidi ya 800 wamekamatwa nchini wakituhumiwa kwa kosa la kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Wanawake hao wamekamatwa kwa kujihusisha na biashara za bangi,mirungi,heroin,cocaine na dawa mpya aina ya methamphetamine kwa mwaka 2023 pekee.

Hata hivyo licha ya Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ya Mwaka 2015 kutoa hukumu ya kifungo kisichopungua miaka 30 kwa kulima bangi au mirungi na kifungo kisichopungua miaka 30 kwa kufanya biashara ,kusafirisha au kukutwa na heroin,methamphetamine au cocaine isiyozidi gramu 200 na kifungo cha maisha ikizidi gramu 200 wanawake hao wameonekana hawaogopi.

Kwa mujibu wa  Taarifa ya Hali ya Dawa za Kulevya ya Mwaka 2023 iliyotolewa Mwezi Mei,2024 na Ofisi ya Waziri Mkuu na Mamlaka ya Kuthibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) imeeleza kuwa operesheni na ukamataji uliofanyika mwaka 2023 ulifanikiwa kukamata dawa za kulevya za mashambani aina ya bangi na mirungi pamoja na dawa za viwandani aina ya heroin,cocaine,methamphetamine na dawa tiba zenye asili ya kulevya.

Taarifa hiyo iliyosaniwa na Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu(Sera,Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama na Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA)Aretas Lyimo imeeleza kuwa jumla ya tani 1965.34 za dawa za kulevya zilikamatwa kwa mwaka 2023 pekee ikiwa ni karibu mara saba zaidi ya kiasi kilichokamatwa tangu Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ianzishwe mwaka 2017.

”Katika mwaka 2023 kiasi cha tani 1757.56 za dawa za kulevya aina ya bangi kilikamatwa kikihushisha watuhumiwa 8,803 kati yao wanaume 8,180 na wanawake 623.

”Mirungi ni dawa ya kulevya ya mashambani ambayo pia imeendelea kuwa tatizo kwa mwaka 2023,jumla ya tani 202.74 ya dawa hii zilikamatwa zikihusisha watuhumiwa 1,179 na kati ya hao wanaume 996 na wanawake 183.

”Mwaka 2023 jumla ya tani 1.31 za dawa za kulevya aina ya heroin ilikamatwa nchini ikihusisha watuhumiw 196 kati ya hao wanaume 168 na wanawake 28”imeleeza taarifa hiyo.

Kwa upande wa dawa za kulevya aina ya cocaine,imefafanuwa kuwa operesheni zilizofanyika mwaka 2023 zilifanikiwa kukamatwa kwa kilo 3.04 za cocaine pamoja na watuhumiwa 32 kati yao wanaume 31 na mwanamke mmoja

‘’Mwaka 2023 jumla ya tani 2.4 za dawa za kulevya aina ya methamphetamine inayotengenezwa kwa kutumia kemikali bashirifu ilikamatwa nchini ikihusisha watuhumiwa tisa katika yao wanaume watano na wanawake wanne’’imeongeza taarifa hiyo.

Hata hivyo sheria Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ya Mwaka 2015  inatoa hukumu ya kifungo cha miaka mitatu au faini ya kuanzia Sh.500,000na isiyopungua Sh.1,000,000 au vyote kwa pamoja kwa kutumia dawa za kulevya.

DCEA inapaswa kupongezwa kwa kazi kubwa iliyoifanya kwa mwaka 2023 na jamii kuipa ushirikiano wa hali juu ili kutokomeza biashara hiyo na hali  ingekuwaje ikiwa tani hizo na watuhumiwa hao wasingekamatwa.

 

Next Post
Gwaride la heshima kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Gwaride la heshima kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi

Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi

Meja Jenerali Mstaafu Semfuko:Watanzania changamkieni fursa ya ufugaji wanyamapori

Meja Jenerali Mstaafu Semfuko:Watanzania changamkieni fursa ya ufugaji wanyamapori

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In