• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Rais Dkt. Samia aagiza kutengenezwa muongozo wa kuwatambua machifu na kazi zao

Kupewa rungu la kuwachongea viongozi wasio waadilifu

by bajeti
July 20, 2024
in Habari
0
Rais Dkt. Samia aagiza kutengenezwa muongozo wa kuwatambua machifu na kazi zao

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, Samia Suluhu Hassan ambae pia ni Kiongozi wa Machifu (Chifu Hangaya) akizungumza na Machifu wa mikoa mbalimbali nchini katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma Julai 20,2024.

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,DODOMA

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan amesema kazi za Machifu katika jamii ni kusuluhisha au kuleta suluhu.

Amesema na pale inapobidi adhabu ipite basi iwe adhabu inayoendana na misingi ya haki kama ilivyo kwenye jamii.

Rais Dkt Samia ametoa kauli hiyo Ikulu Chamwino jijini Dodoma Julai 20,2024 wakati akizungumza na Machifu kutoka mikoa mbalimbali nchini.

Rais Dkt.Samia ambaye pia ni Kiongozi wa Machifu nchini anayejulikana kama Chifu Hangaya amebainisha kuwa kila wanapokwenda mahali  wanakutana na  malalamiko mengi ya wananchi na anapotokea kiongozi wa chama au Serikali ndio wananchi wanakimbilia.

‘’Tunaomba machifu tusaidieni, nyinyi kama viongozi wa jamii mliokubalika kule,migogoro mingine hii tusaidieni.

‘’Migogoro  mingi katika jamii zetu inakiuka mila na heshima za watu,jengeni mvuto kwa watu wetu waje wawakimbilie pamoja na tofauti za wanajamii lakini wote tuhakikishe tunawaongoza watu kwa maridhiano kwenye mambo tofauti tustahimiliane tufanye mabadiliko na tusonge mbele’’amesema Rais Dkt Samia (Chifu Hangaya)

Rais Dkt Samia(Chifu Hangaya) ameongeza kuwa  Machifu wanadhamana ya Sheria za Kimila na wanapowaita watu na kuwahukumu kwa Sheria za Kimila watu huwa hawarudi nyuma.

‘’Sisi ndio tunaifanya jamii iheshimu misitu yetu kwani huko ndiko tunakokwenda kuomba lakini kwa yale maeneo ambayo Machifu hawafanyi kazi hii ni kukame, hakuna baraka na mvua hazinyeshi.

‘’Niliwaelekeza  Wizara watengeneze muongozo ambao utawatambua Machifu na mambo yao wanayoyafanya katika maeneo yao.

‘’Kama mnamuona kiongozi  haendi mwendo mwema tuambieni tumjue ili tulete viongozi waadilifu na mambo yaende vizuri”amesema Rais Dkt Samia (Chifu Hangaya)

 

Next Post
Wanawake zaidi ya 800 wakamatwa wakijihushisha na biashara ya dawa za kulevya

Mikoa 12 wanawake waongoza matumizi dawa za kulevya,Njombe ‘ngoma droo’

Watanzania watakiwa kulinda amani,matunda yake yanawafaidisha wote

Watanzania watakiwa kulinda amani,matunda yake yanawafaidisha wote

Tani dawa za kulevya ‘zautikisa’ mwaka 2023.

‘Mapapa’ wa dawa za kulevya sasa yatumia drone,mitandao ya kijamii

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:5
  • Today's page views 5
  • Total visitors 13,061
  • Total page views 14,806

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In