• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma(PPAA) kutoa elimu kwa wazabuni

by bajeti
September 12, 2024
in Habari
0
Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma(PPAA) kutoa elimu kwa wazabuni

Katibu Mtendaji wa Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA), James Sando akizungumza na waandishi wa Habari (hawapo pichani) pembezoni mwa Kongamano la 16 la Ununuzi wa Umma la Afrika Mashariki Jijini Arusha Septemba 12,2024(Picha na mpigapicha wetu)

Share on FacebookShare on Twitter

 

NA MWANDISHI WETU,ARUSHA

MAMLAKA ya Rufani ya Zabuni za Umma Tanzania (PPAA) imejipanda kutoa elimu kwa wazabuni katika kanda zote nchini ikiwa ni jitihada za kuwafikia wadau wa ununuzi wa umma hususan wazabuni

Hayo yamezungumzwa mbele ya waandishi wa habari Septemba 12,2024 jijini Arusha pembezoni mwa Kongamano la 16 la Ununuzi wa Umma la Afrika Mashariki na  Katibu Mtendaji wa Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA),James Sando

Sando amesema Mamlaka imeweka mkakati huo ili kuweza kuzifikia kanda nne  ambazo hazijapatiwa elimu ya jinsi ya kuwasilisha mashauri yao pale ambapo hawakuridhishwa na mchakato wa ununuzi.

“Mkakati tulio nao katika mwaka huu wa fedha 2024/25 ni kuhakikisha kuwa tuwafikia wazabuni katika kanda nne ambazo hatujazifikia, katika kufika kwetu katika Kanda hizo tutakuwa tumewafikia wazabuni wengi,” amesema Sando

Sando amezitaja Kanda hizo kuwa ni Kanda ya Kati, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini na Kanda ya Kusini.

Wakati huohuo, Naibu Katibu Mtendaji wa PPAA, Florida Mapunda amezitaja faida za kuanzishwa kwa moduli ya kuwasilisha rufaa/malalamiko kwa njia ya kieletroniki na kueleza kuwa imesaidia kupunguza gharama na muda.

“Moduli hii itasaidia kupunguza gharama na muda kwa kuwa utaratibu wa zamani ulikuwa unamlazimu mzabuni kuwasilisha malalamiko yake katika ofisi za Mamlaka ya Rufani,”ameongeza Mapunda

Aidha amebainisha kuwa  Moduli hii itamwezesha mzabuni au mfanyabiasha kuona hatua kwa hatua jinsi rufaa yake inavyoshughulikiwa hadi utoaji wa hukumu na kuongeza kuwa italeta uwazi na uwajibikaji na hivyo kuwapa imani wazabuni ya kuamini katika mifumo ya utoaji haki kwenye michakato ya zabuni za umma.

Kongamano la Wadau wa Ununuzi wa Umma limewakutanisha wadau wa ununuzi wa ndani ya Tanzania na Nje zaidi ya 1,500. Kauli mbiu ya kongamano hilo ni: “Matumizi ya Dijitali kwa Ununuzi wa Umma Endelevu.

 

 

Next Post
Makamu wa Rais Dkt. Mpango ahimiza Upandikizaji Mimba katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kuwa endelevu

Makamu wa Rais Dkt. Mpango ahimiza Upandikizaji Mimba katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kuwa endelevu

Hizb ut Tahrir / Tanzania yalaani mauaji ya Kibao

Hizb ut Tahrir / Tanzania yalaani mauaji ya Kibao

Japan na Tanzania kuimarisha ushirikiano

Japan na Tanzania kuimarisha ushirikiano

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In