• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

TARI yatoa mafunzo kwa Wakulima na Maafisa Ugani 165

Yashirikiana na watafiti kutoka icipe

by bajeti
September 14, 2024
in Mazingira
0
TARI yatoa mafunzo kwa Wakulima na Maafisa Ugani 165

Wakulima wa mchaungwa kutoka Wilaya ya Muheza mkoani Tanga(majina yao hayajafahamika) wakiwasikiliza Watafiti kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI) juu ya kudhibiti wadudu waharibifu wa machungwa Septemba 9,2024(Picha na mpigapicha wetu)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,KILIMANJARO

TAASISI ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kwa kushirikiana na watafiti kutoka Kituo cha Kimataifa cha Utafiti wa Fiziolojia na Ikolojia ya Wadudu (icipe) kutoka nchini Kenya imetoa mafunzo kwa maafisa ugani na wakulima viongozi 165 juu ya njia husishi za kudhibiti wadudu waharibifu wa matunda ya Parachichi, Machungwa na Embe.

Mafaunzo hayo yametolewa kupitia vituo vya utafiti vya Ukiriguru (Mwanza), Tengeru (Arusha) na Mlingano (Tanga) kwa maafisa ugani na wakulima viongozi 165 kutika Kata 31  za maeneo hayo

Awali akifungua mafunzo hayo Septemba 9 hadi 13, 2024  wilayani Hai mkoani Kilimanjaro, Mkuu wa Wilaya hiyo Lazaro Twange ameipongeza TARI kwa kuweka nguvu ya kuwajengea uwezo wataalam wa kilimo na wakulima viongozi katika maeneo mbalimbali ikiwa ni sehemu ya juhudi za serikali kuinua sekta hiyo muhimu.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Muheza Dkt. Juma Mhina amebainisha kuwa  mradi huo umekuja wakati sahihi na kwa watu sahihi akitolea mfano wa Muheza kuwa uchumi wa wananchi wa wilaya hiyo hutegemea machungwa na wamekuwa na kilio cha wadudu waharibifu wa matunda hayo.

Aidha Dkt. Mhina amesema mradi huo utakuwa ni suluhisho la changamoto ya wadudu waharibifu huku ikichangia kipato cha wakazi wa Muheza, kuongezeka mapato ya Halmashauri na hatimaye taifa kwa ujumla kupitia kilimo cha matunda yanayouzwa ndani na nje ya nchi.

Mtafiti Kiongozi wa Mradi huo kutoka TARI Ukiriguru Dkt, Abdullah Mkiga amesema lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha wakulima  wanapata elimu bora ya kudhibiti wadudu waharibifu wa matunda kama Nzi na Nondo wanaoshambulia matunda na kusababisha matunda kuoza na kushusha kiwango cha mavuno na ubora.

Kwa upande wake Mtafiti kutoka ICIPE Dkt. Shepard Ndlela amesema kupitia njia husishi za kudhibiti visumbufu mkulima ataweza kupunguza gharama na matumizi ya viuadudu vya kemikali na kuongeza mavuno na ubora kwa soko ndani na kimataifa.

Maafisa Ugani wakiendelea kufutilia mafunzo juu ya kuthibiti wadudu waharibifu wa machungwa na parachichi wilayani Hai Mkoa wa Kilimanjaro yaliyotolewa na Kituo cha Utafiti wa Kilimo (TARI) Septemba 12,2024.(Picha na mpigapicha wetu)

Akizungumzia kuhusu mafunzo hayo,Mkulima wa machungwa wa Kijiji cha Mkinga Wilaya ya Muheza mkoani Tanga Fatuma Muhammed amesema mafunzo hayo yamewasaidia sio tu kutambua wadudu waharibifu bali pia kutambua wadudu rafiki kwenye uzalishjai wa matunda ambao awali walidhani ni hatarishi lakini Wataalamu wamewaeleza ni wadudu rafiki wanaozuia wadudu waharibifu kushambulia matunda na wanachangia kuongeza tija.

“Sisi tulijua hawa wadudu (jamii ya siafu) tunawaita huku kwetu “madadada” kuwa ni waharibifu wa machungwa lakini wataalamu wametueleza ni wadudu rafiki wanaozuia wadudu wengine kushambulia machungwa” amesema Mohammed

Mafunzo hayo yamefanyika katika Wilaya za Hai, na Siha Mkoa Kilimanjaro na Muheza, mkoani Tanga ikiwa ni utekelezaji wa mradi wa njia husishi za kudhibiti wadudu wa miti ya matunda kwenye ikolojia mbalimbali (Fruit tree agro ecological-based IPM).

Katika Wilaya za Hai na Siha mafunzo hayo yalijikita katika matunda ya parachichi, huku kwa Wilaya ya Muheza yakijikita kwenye matunda ya machungwa na embe.

Mradi wa ‘Fruit tree agro ecological-based IPM’ unatekelezwa kwa miaka mitatu (2023-2026) kupitia kituo cha TARI Ukiriguru kwa kushirikiana na Taasisi ya ICIPE chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ).

 

 

Next Post
INEC yawaasa watendaji wake kuwa makini

INEC yawaasa watendaji wake kuwa makini

Polisi yachunguza kifo cha Daktari aliyekutwa amefariki

Polisi yachunguza kifo cha Daktari aliyekutwa amefariki

Russia yatishia kuligeuza Jiji la Kiev,Ukraine kuwa’’ lundo lililoyeyushwa’’

Russia yatishia kuligeuza Jiji la Kiev,Ukraine kuwa’’ lundo lililoyeyushwa’’

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:5
  • Today's page views 5
  • Total visitors 13,061
  • Total page views 14,806

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In