• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Polisi yachunguza kifo cha Daktari aliyekutwa amefariki

aacha ujumbe kwa mkewe,

by bajeti
September 15, 2024
in Habari
0
Polisi yachunguza kifo cha Daktari aliyekutwa amefariki

Hayati Dkt. Dismas Dominic (Chami) enzi za uhai wake

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,DODOMA

JESHI  la Polisi kwa kushirikiana na wataalam wengine wa uchunguzi, linachunguza kifo cha Daktari Dismas Dominic  (Chami 32), mkazi wa Ulyankulu aliyekuwa  anafanya kazi katika Kituo cha Afya Ulyankulu ambaye amekutwa amefariki dunia huko katika eneo la Kombo Masai Kata ya Malolo Mkoa wa Tabora.

Kwa mujibu wa taarifa ya iliyotolewa Septemba 15,2024 na Msemaji wa Jeshi la Polisi jijini Dodoma  DCP David Misime amesema mwili wake umekutwa ukiwa na dripu yenye dawa ambayo haijafahamika mkononi.

Amesema Daktari huyo alimuaga Mkuu wake wa kazi na mke wake Septemba 2,2024 kuwa, anaelekea Tabora kushughulikia akaunti yake ya benki iliyokuwa na changamoto na angelirejea Septemba 3,2024.

‘’Septemba 4,2024 hakupatikana kupitia mawasiliano yake ya simu. Septemba 10,2024 Daktari Mkuu wa Kituo hicho cha afya akiambatana na mke wa Dkt. Dismas Dominic (Chami) walifika katika kituo cha Polisi na kutoa taarifa ya kutokuonekana kwake toka Septemba 2,2024.

‘’Tarehe hiyo hiyo Dkt. Dismas Dominic (Chami) alimtumia ujumbe mke wake kwa njia ya Whatsapp unaosema

“Nisamehe sana baada ya dakika chache sitakuwa nanyi duniani,simamia kila kitu nilichoanzisha pesa zote zipo akaunti ya CRDB simamia na watoto wa some kwa heri”.amesema DCP Misime

DCP Misime ameongeza kuwa baada ya ujumbe huo hakupatikana tena hadi alipopatikana Septemba 13,2024 majira ya saa tatu usiku akiwa amefariki dunia

‘’Uchunguzi wa awali umebaini kuwa, alishajaribu kujiua mara mbili’’amebainisha DCP Misime

 

Next Post
Russia yatishia kuligeuza Jiji la Kiev,Ukraine kuwa’’ lundo lililoyeyushwa’’

Russia yatishia kuligeuza Jiji la Kiev,Ukraine kuwa’’ lundo lililoyeyushwa’’

TFC yakabidhi tani 61,000 za mbolea ya rukuzu

TFC yakabidhi tani 61,000 za mbolea ya rukuzu

DCEA yamnasa wakala wa dawa za kulevya Tanzania,yumo bibi wa miaka 70

'Mapapa' wa biashara dawa za kulevya wahamia kwenye vyakula vinavyopendwa na watoto

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In