• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Kongamano la Kimataifa kujadili Tasnia ya Mbolea kufanyika Dodoma

Kuwakutanisha washiriki zaidi ya 250 wa ndani na nje ya nchi

by bajeti
October 1, 2024
in Habari
0
Kongamano la Kimataifa kujadili Tasnia ya Mbolea kufanyika Dodoma

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Joel Laurent (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuelekea maadhimisho ya Siku ya Mbolea Duniani yatakayofanyika kitaifa mkoani Manyara.Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ruzuku Kitaifa Louis Kasera.(Picha na TFRA)

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO

KONGAMANO la Kimataifa la kujadili Tasnia ya Mbolea  nchini linatarajiwa kufanyika jijini Dodoma na kuwakutanisha zaidi ya washiriki 250 kutoka ndani na nje ya Tanzania.

Kongamano hilo linaloelezewa kuwa la aina yake litafanyika Oktoba 11 na 12,2024 jijini humo kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mbolea Duniani inayoadhimishwa kila mwaka ifikapo Oktoba 13.

Hayo yameelezwa Oktoba 1,2024 mkoani Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Joel Laurent wakati akizungumza na waandishi wa habari

Amesema kongamano hilo litawakutanisha pamoja wadau wa Tasnia ya Mbolea  kitaifa na kimataifa na linatarajiwa kuja na majibu ya changamoto inayoikabilia tasnia hiyo na wakulima kwa ujumla

‘’Kongamano hilo litahidhuriwa na washiriki takribani 250 kutoka ndani na je ya nchi watakaojadili mada mbalimbali kuhusu Tasnia ya Mbolea kwa ujumla wake.

‘’Hii itatoa fursa kwa wadau hao kujadili kwa pamoja mabadiliko chanya ya Tasnia ya Mbolea,kubadilishana uzoefu na kujadili namna bora ya kutatua changamoto zinazoikabilia tasnia hiyo

‘’Mada zinakazojadiliwa ni pamoja na usimamizi na udhibiti wa mbolea,mchango wa afya ya udongo katika kuimarisha usalama wa chakula nchini ikiwemo matumizi ya Tehama katika kusimamia Tasnia ya Mbolea’’amesema Laurent

Laurent amefafanuwa kuwa wakati Kongamano hilo likiendelea ,mkoani Manyara maadhimisho hayo yataendelea kuanzia Oktoba 10,11 na 12,2024 na yatahusisha maonesho  kutoka kwa wadau mbalimbali wa Sekta ya Kilimo

‘’Lengo la maadhimisho ya Siku ya Mbolea Duniani ni kupanua wigo wa kuelezea masuala mbalimbali katika tasnia hiyo ikiwemo mafanikio yake nchini,kutoa elimu kwa wadau,hususani wakulima na wafanyabiashara,na kauli mbiu kwa nwaka 2024 ni ‘’Tuongee Mbolea,Kilimo ni Mbolea

‘’Kauli mbiu hii inaenda mbamba na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kuthamini umuhimu wa mbolea katika Sekta ya Kilimo ambako kwa misimu mitatu mfululizo Serikali imeendelea kuwanufaisha wakulima kwa kuweka ruzuku kwenye mbolea’’ameongeza Laurent

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Ruzuku Kitaifa Louis Kasera amesema hadi sasa zaidi ya wakulima Milioni nne wamesajiliwa katika mfumo wa ruzuku ya mbolea  ambao umesaidia pia kuondoa mbolea feki.

 

Next Post
Ushirikiano wa Tanzania na Falme za Kiarabu (UAE) wazidi kuimarika

Ushirikiano wa Tanzania na Falme za Kiarabu (UAE) wazidi kuimarika

Benki ya Dunia yaridhishwa utekelezaji miradi ya maji Pangani

Benki ya Dunia yaridhishwa utekelezaji miradi ya maji Pangani

Makamu wa Rais Dkt.Mpango kufungua Mkutano wa 53 wa Mwaka wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika

Makamu wa Rais Dkt.Mpango kufungua Mkutano wa 53 wa Mwaka wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 13,062
  • Total page views 14,807

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In