• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Makala

Kuelekea Siku ya Mbolea Duniani: Vijana wachangamkia ukuzaji biashara ya mbolea

kupitia Programu ya Jenga Kesho iliyo Bora (BBT),Vijana na Wanawake wapewa mafunzo na TRFA

by bajeti
October 3, 2024
in Makala
0
TFRA:Matumizi ya mbolea yafikia tani 840,000 mwaka 2023/2024

Baadhi ya Vijana waliofuzu mafunzo ya uendeshaji wa biashara ya mbolea wa Programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (Building a Better Tomorrow - BBT) wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Joel Laurent hayupo (pichani) kabla ya kutunukiwa vyeti na Mamlaka hiyo wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma Septemba 22,2024.(Picha na TFRA)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,TFRA

OKTOBA 13,  2024 Tanzania itaungana na mataifa mengine Ulimwenguni  kuadhimisha Siku ya Mbolea Duniani, ambapo mchango wa vijana na wanawake katika kuimarisha biashara ya mbolea litakuwa moja ya maeneo yanayofanyiwa tathmini ya kina ili kuhamasisha harakati za kukuza sekta mama ya kilimo.

Katika kipindi cha miaka mitatu ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassani, madhimisho ya Siku ya Mbolea Duniani yametumika kwa wadau mbalimbali wa kilimo, wakiwemo vijana na wanawake, kutathmini mchango wa mbolea katika uzalishaji wa mazao mbalimbali ya chakula na biashara.

Kupitia jukwaa hili la Siku ya Mbolea, Mamlaka ya Udhibiti Mbolea Tanzania (TFRA) ni moja ya taasisi ambazo zimekuwa mstari wa mbele katika kukuza na kuongeza ajira zenye staha na ushiriki wa vijana na wanawake kwenye kilimo.

Kwa kupitia Programu ya Jenga Kesho iliyo Bora (BBT), TFRA imetoa mafunzo ya elimu ya biashara ya mbolea kwa vijana na wanawake ikiwa ni mchango wake unaolenga kuongeza ajira za staha, kuongeza tija, kubakiza wakulima kwenye sekta na kupunguza umasikini.

Wakulima, Watunga Sera na Watoa Maamuzi wanapojiandaa kusheherekea Siku ya Mbolea Duniani wanalishukuru Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuanzisha Programu ya BBT ikiwa na malengo manne ya kuongeza ajira, mitaji, teknolojia na umilikishwaji wa ardhi.

Programu hiyo inatekelezwa kupitia miradi minne ambayo ni mashamba makubwa ya pamoja, utoaji wa mikopo yenye riba nafuu, visima kwa wakulima wadogo na ugani.

Programu hiyo ambayo inahesabika kama mkombozi kwa maelfu ya vijana na wanawake ilizinduliwa rasmi na Rais Dkt.Samia mwezi Machi mwaka  2023.

Kwa mujibu wa Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, hadi kufikia Aprili mwaka huu 2024, jumla ya ekari 340,465.28 zimeshapatikana kwa ajili ya programu ya BBT mikoa ya Dodoma, Kigoma, Mbeya, Singida, Pwani, Tanga, Njombe na Kagera.

Katika kuimarisha ushiriki wa vijana na wanawake katika  programu hii, Wizara ya Kilimo imetoa mafunzo kuhusu kilimo biashara na kuwapatia mashamba.

Ni katika programu hii ya mafunzo ya elimu biashara ya mbolea,Mkurugenzi Mtendaji wa TFRA, Joel Laurent, hivi karibuni aliwakabidhi vyetu vijana 192 wa BBT waliohitimu mafunzo hayo.

Mafunzo ya vijana hao yalifanyika katika shamba lao la Chinangali II wilayani Chamwino, Mkoa Dodoma.

Vyeti walivyokabidhiwa vijana hao vitawasaidia kujisajili kuwa mawakala wa pembejeo za mbolea ambapo jumla ya ekari 5,700 kati ya ekari 11,430 katika shamba la Mlazo/Ndogowe zimesafishwa na visima 12 na mabwawa matano yamechimbwa kwa ajili ya kuhifadhi maji ya umwagiliaji.

Mbali na hilo lakini pia  jumla ya ekari 1,000 katika shamba hilo zimetengwa kwa ajili ya kuwapatia wanakijiji wanaolima kulizunguka shamba hilo.

Hali kadhalika, nyumba 53 zimejengwa katika shamba hilo kwa ajili ya vijana na wanawake wa BBT.

Kwa kutambua umuhimu wa miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Wizara ya Kilimo, TFRA iliratibu mafunzo kwa vijana 192 kwa kushirikiana na Idara ya Mafunzo ya Wizara ya Kilimo kupitia Vyuo Vya Mafunzo (MATI) ili kutoa mafunzo ya uendeshaji wa biashara ya mbolea kwa kuzingatia Sheria ya Mbolea Na. 9 ya mwaka 2009.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Joel Laurent akimkabidhi cheti mmoja wa vijana kati ya 192 cha kuhitimu mafunzo ya uendeshaji wa biashara ya mbolea wa Programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (Building a Better Tomorrow – BBT) Septemba 22,2024 wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma.(Picha na mpigapicha wetu)

Akizungumza na vijana hao wakati wa zoezi la ugawaji vyeti,Mkurugenzi Mtendaji  wa TFRA Joel Laurent anasema matumizi ya mbolea yameongezeka kutoka 500,000 kwa mwaka 2022/2023 hadi kufikia tani 840,000 mwaka 2023/2024.

Anasema Ongezeko hilo lilichagizwa na ruzuku ya mbolea iliyotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan.

“Ongezeko la matumizi ya mbolea ni kubwa; hii inaashiria namna jamii ilivyoelimika na kutambua umuhimu kwenye shughuli za kilimo,” anasema na kuendelea: “ TFRA inaendelea kupanua wigo wa utoaji elimu ya matumizi sahihi ya mbolea kwa wakulima ili waendelee kunufaika.”anaongeza Laurent

Laurent anawapongeza vijana waliomaliza mafunzo yao kwa kuwa yatawajenga katika Sekta ya Kilimo waliyoichagua kama nguzo ya uchumi wao.

Aidha anabainisha kuwa mafunzo yaliyotolewa kwao yana maana zaidi kwa maandalizi ya msimu ujao wa kilimo wa 2024/2025.

Mkurugenzi huyo wa TFRA pia ameishukuru Wizara ya Kilimo kwa kuwalea vijana wa BBT, hatua ambayo inasaidia katika ukuaji wa sekta mama ya kilimo.

Naye Mratibu wa Mradi wa BBT, Mathed Kahaya, anaishukuru TFRA kwa kutoa mafunzo hayo kwa vijana akisema ni lazima wayazingatie ili waweze kunufaika katika shughuli zao za kilimo.

Next Post
Kiruavunjo:wamshukuru Rais Dkt.Samia kuwapelekea miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira

Kiruavunjo:wamshukuru Rais Dkt.Samia kuwapelekea miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira

Kamishna Jenerali Lyimo:Tutavunja mitandao yote mikubwa ya dawa za kulevya

Sababu waraibu dawa za kulevya kuharibika sura ‘kulala wakiwa wamesimama’

IGP Wambura atembelea Kigoma kuangalia hali ya usalama

IGP Wambura atembelea Kigoma kuangalia hali ya usalama

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In