• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, January 18, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Kila halmashauri Tanzania kuwa na msitu wake wa asili

lengo ni halmashauri hizo kuingia kwenye biashara ya Kaboni

by bajeti
October 24, 2024
in Mazingira
0
Kila halmashauri Tanzania kuwa na msitu wake wa asili

Wananchi wa Kijiji cha Mwaboza, Kata ya Moa katika Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Ashatu Kijaji (hayupo kwenye picha) juu ya utunzaji wa mazingira wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua, kuweka mawe ya msingi na kukagua miradi ya maendeleo na kufanya mikutano ya kuongea na wananchi, Oktoba 23,2024.

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,TANGA

SERIKALI inaandaa mpango wa kuongeza misitu ya asili kwa kila halmashauri nchini kuwa na msitu wake ikiwa moja ya njia ya Uhifadhi na Utunzaji wa Mazingira utakaosaidia katika biashara ya kaboni.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Ashatu Kijaji ameyasema hayo Oktoba 23,2024 wilayani Kilindi Mkoa wa Tanga wakati  wa ziara yake ya kikazi ya kukagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi ya maendeleo.

Dkt. Kijaji ameeleza kuwa lengo ni halmashauri hizo ni kuingia kwenye biashara ya Kaboni ambapo zoezi la kupandwa miti kwa pamoja litawezesha faida kuonekana haraka kuliko kupandwa na mtu mmoja mmoja.

Aidha ameongeza mpango huo utashirikisha hasa wale ambao wana maeneo makubwa ya ardhi ambapo wanaweza kutumia ekari tano hadi 10 kwa ajili ya kupanda miti hiyo.

“Kufanikiwa kwa kupandwa miti hiyo kutasaidia kupunguza athari za mabadiliko ya tabia nchi ambayo mengine yanasababisha ongezeko la joto pamoja na mvua ambazo hazina mpangilio mzuri,” amesema.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt. Batilda Burian amesema kumekuwepo na changamoto ya wananchi kuchoma misitu hovyo na hivyo wamekuwa wakiendelea kutoa elimu kwa wananchi kuona jinsi ya kuzuia matukio hayo.

Ameeleza kuwa mkoa huo una zaidi ya hekta 700,000 za misitu ambapo ndani yake kuna mashamba matatu ya miti lakini kumekuwa na changamoto ya wananchi kuvamia na kuingiza mifugo pamoja na kuchoma mkaa, ambapo  mamlaka husika zinaendelea na udhibiti.

Amesisitiza kuwa katika mkoa huo wananchi pia wamekuwa wakijishughurisha na kilimo cha mikoko ambacho kinasaidia katika utunzaji wa mazingira ya bahari kwani wakati wa mmomonyoko wa udongo miti hiyo inasaidia kusitokee uharibifu kwenye maeneo ambapo mikoko ipo.

 

Next Post
Dkt.Mpango ataka matumizi ya ndoo kama choo magerezani kuondolewa

Dkt.Mpango ataka matumizi ya ndoo kama choo magerezani kuondolewa

BRELA yatekeleza agizo la Rais Dkt.Samia kuhusu Mifumo ya Kitaasisi kusomana

BRELA yatekeleza agizo la Rais Dkt.Samia kuhusu Mifumo ya Kitaasisi kusomana

TARI,ZARI na NIBIO wajadili  Afya ya Udongo

TARI,ZARI na NIBIO wajadili Afya ya Udongo

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:27
  • Today's page views 27
  • Total visitors 13,184
  • Total page views 14,930

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In