• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Sayansi na Teknolojia

BRELA yatekeleza agizo la Rais Dkt.Samia kuhusu Mifumo ya Kitaasisi kusomana

Lengo ni kurahisisha utoaji wa huduma kwa njia ya mtandao

by bajeti
October 27, 2024
in Sayansi na Teknolojia
0
BRELA yatekeleza agizo la Rais Dkt.Samia kuhusu Mifumo ya Kitaasisi kusomana
Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

AFISA Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Godfrey Nyaisa  amesema Taasisi hiyo kwa  sasa imetekelea agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan juu ya kuhakikisha  Mifumo yote ya Kitaasisi inasomana.

Nyaisa ametoa kauli hiyo Oktoba 25,2024 mkoani Dar es Salaam katika ufunguzi wa mkutano wa pili wa Taasisi hiyo na wadau wake.

Amesema lengo ni kurahisisha utoaji wa huduma kwa njia ya mtandao na kuondoa usumbufu usio wa lazima kwa wananchi ikiwa ni pamoja na wafanyabiashara kwa ujumla.

‘’Urasimishaji wa biashara ni mchakato kwa maana ya “process”,Usajili aidha wa Kampuni au Jina la Biashara ni sehemu ya mchakato tu wa Urasimishaji wa biashara.

‘’Mara baada ya kusajili Mfanyabiashara anatakiwa kupata leseni au vibali kutoka Mamlaka nyingine za Serikali ikiwa ni pamoja na Namba ya Utambulisho wa Mlipa Kodi (TIN), Leseni ya Biashara na Vibali kutoka Mamlaka za Uthibiti “Regulatory Authorities”amesema Nyaisa

 Amesema kwa namna ya kipekee ametambua uwepo wa Taasisi dada kutoka upande wa Zanzibar; Wakala wa Usajili wa Biashara na Mali (BPRA) wanaotoa huduma sawa na BRELA, na Ofisi ya Hakimiliki Zanzibar (COSOZA) wanaotoa huduma sawa na COSOTA.

‘’Uwepo wa Taasisi za Umma na Binafsi kwenye Mkutano huu wa pili wa BRELA na wadau wake utasaidia kujadili mafanikio, fursa na changamoto za Sekta ya Biashara.

‘’Kauli Mbiu ya Mkutano wa Mwaka huu ni “Mifumo ya Kitaasisi inayosomana na Uwezeshaji wa Biashara nchini” (Interoperability of Institutional Systems and Business Facilitation),wote ni mashaidi kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mama yetu Mpendwa Samia Suluhu Hassan, amekuwa akitoa maelekezo na miongozo ya Mifumo ya Taasisi za Serikali kusomana.

‘’Lengo ni kurahisisha utoaji wa huduma kwa njia ya mtandao na kuondoa usumbufu usio wa lazima kwa wananchi ikiwa ni pamoja na wafanyabiashara kwa ujumla’’amefafanuwa Nyaisa

 Aidha ameongeza  kuwa mageuzi makubwa yalianza kufanyika Desemba 3, 1999, baada ya BRELA kuwa Wakala wa Serikali chini ya Sheria ya Wakala za Serikali “Executive Agency Act No. 30 of 1997” ambapo mabadiliko haya yalilenga kuharakisha utoaji huduma na kuboresha mazingira ya utendaji kazi.

‘’Mwaka 2015 BRELA ilianzisha mfumo wa kwanza wa usajili wa Majina ya Biashara kwa njia ya Mtandao “Online Business Name Registration System – OBRS” ambapo mfumo huo ulitengenezwa na watumishi wa BRELA kwa kushirikiana na vijana wengine wakitanzania na Januari 4, 2018, BRELA ilianza kutumia mfumo mpya wa Usajili kwa Njia ya Mtandao “Online Registration System- ORS”, mfumo huu unatoa huduma zote za sajili na za baada ya sajili “Registration and Post Registration” zikiwa ni pamoja na sajili za Makampuni, Majina ya Biashara, Alama za Biashara na Huduma, Hataza pamoja na Leseni za Viwanda.

‘’Kwa upande wa Leseni za Biashara za Kundi “A” zilizohamishiwa BRELA kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara pia zinatolewa kwa njia ya Mtandao kupitia Mfumo wa “Tanzania National Business Portal – TNBP”.

‘’Huduma hizi zimerahisisha sana wateja kupata huduma popote pale walipo, huduma nyingine zikiwa ni kwa siku moja tu ambapo kabla ya mifumo hii kuanza wateja walikuwa wanalazimika kutoka sehemu zote za nchi kuja kupata huduma Dar es Salaam huku huduma nyingine  zikigharimu kiasi cha Sh. 1,000 lakini wateja walilazimika kutoka Mbeya, Arusha, Mwanza, Rukwa na mikoa mengine kufuata huduma hii”amesema Nyaisa

 Nyaisa ameeleza kuwa Mfumo huo wa ORS umetimiza miaka sita,na ni dhairi teknolojia na baadhi ya sheria zimebadilika sana.

‘’Hivyo, sisi kama BRELA tulishaanza maboresho ya Mfumo huo kwa kuufanya uwe bora na rafiki zaidi, nikiri kuwa katika mfumo wa sasa kuna baadhi ya taarifa zinazolazimu kujazwa zaidi ya mara moja, kitu ambacho mfumo ungeweza kuvuta taarifa hizo bila kuhitaji kujazwa tena. Zoezi la maboresho lilishirikisha maoni ya wadau kwani wao ndiyo watumiaji wakubwa wa Mfumo huu.

‘’Maboresho haya yamezingatia uwepo wa huduma zingine, mfano upande wa Leseni za Biashara, BRELA inaendelea na mashauriano na mamlaka zingine ili kutumia mfumo mmoja wa Leseni za Biashara utakao kuwa na uwezo wa kutoa Leseni za Kundi “A” zinazotolewa na BRELA na Leseni za Kundi “B” zinazotolewa na Serikali za Mitaa “Local Government Authorities” bila kuathiri mapato ya Halmashauri husika.’’amebainisha Nyaisa

Aidha Nyaisa ameishukuru Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kusimamia kwa dhati majadiliano ya kuwa na mfumo mmoja wa utoaji Leseni za Biashara na Uanzishwaji wa mfumo huo mmoja wa Leseni utaisaidia sana Serikali kwenye takwimu pamoja na kuthibiti upotevu wa mapato kwa kuondoa leseni za kuandikwa kwa mikono.

 

Next Post
TARI,ZARI na NIBIO wajadili  Afya ya Udongo

TARI,ZARI na NIBIO wajadili Afya ya Udongo

Serikali yapeleka mamilioni ya fedha kuimarisha kitengo cha maabara na mifupa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini Mtwara

Serikali yapeleka mamilioni ya fedha kuimarisha kitengo cha maabara na mifupa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini Mtwara

VETA yaanzisha kozi kwa wafanyakazi wa majumbani (house girl/boy)

VETA yaanzisha kozi kwa wafanyakazi wa majumbani (house girl/boy)

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In