• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Serikali yapeleka mamilioni ya fedha kuimarisha kitengo cha maabara na mifupa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini Mtwara

Yahudumia mikoa mitatu na nchi jirani za Msumbuji na Visiwa vya Comoro

by bajeti
November 5, 2024
in Habari
0
Serikali yapeleka mamilioni ya fedha kuimarisha kitengo cha maabara na mifupa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini Mtwara

Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini Mtwara ikionekana kwa nje.(Picha na Goodluck Hongo)

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO,MTWARA

SERIKALI imeendelea kupeleka mabilioni ya fedha katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini-Mtwara (Mitengo) ambapo sasa mgonjwa haitaji kuwa na rufaa ili apate  huduma za kibingwa za madaktari bingwa.

Mbali na hiyo lakini kwa sasa hospitali hiyo mpya inayohudumia mikoa ya Lindi,Mtwara na Ruvuma zikiwemo nchi jirani za Msumbuji na Visiwa vya Commoro ina uwezo wa kuotesha sampuli na kubaini vimelea na  dawa gani ya kutibu vimelea hivyo

 

Jengo la Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini Mtwara kama inavyoonekana kwenye wa nje

Akizungumza na Bajeti Communication Oktoba 28,2024 mkoani Mtwara waliotembelea hospitali hiyo kujionea uwekezaji wa Serikali uliofanyika katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya,Mkuu wa Kitengo cha Maabara katika hospitali hiyo, Shaibu Nanyanga amesema Serikali imetoa fedha nyingi katika kuboresha jengo la maabara,idara ya kemia hai na mikrobiolojia ambapo  vitengo hicvyo vipo ndani ya jengo moja la maabara.

Amesema  kiasi cha zaidi ya Sh.Milioni 240 zilizotolewa zimefanya uwekezaji mkubwa waa kitengo cha maabara kwa kununua mashine za kisasa na  kwa upande wa idara ya kemia hai ambapo awali walikuwa wakitumia mashine ndogo hivyo kuwezesha kitengo hicho kupima sampuli za aina mbalimbali na kutoa majibu ya haraka..

‘’Kwa sasa tunauwezo wa kupima sampuli zaidi ya 600 kwa wakati mmoja na kutoa majibu kwa haraka kwa wateja wetu’’amesema Nanyanga

Mkuu wa Kitengo cha Maabara katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini Mtwara Shaibu Nanyanga akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) Oktoba 28,2024 vifaa vya kisasa vilivyonunuliwa na Serikali kwa ajili ya kuboresha na kukiongezea uwezo kitengo cha maabara cha hospitali hiyo ili kiweze kutoa huduma bora kwa wananchi(Picha na Bajeti Communication)

 

Akizungumzia uwekezaji uliofanyika upande wa Mikrobiolojia(Maabara ya kuoteshavimelea vinavyosababisha  magonjwa katika mwili wa mwanadamu), Nanyanga amefafanua kuwa Serikali ilipeleka fedha kiasi cha Sh.Milioni 108 ili kuimarisha uwezo wa maabara hiyo ambapo kwa sasa inauwezo wa kuotesha sampuli zote za kibaiolojia ikiwemo mkojo,damu na vingine.

‘Idara ya Mikrobiolojia ni idara muhimu sana  kwa utoaji huduma kwa wateja wetu  na tunaamini kwa uwekezaji uliofanyika katika idara hii utaturahisishia kwa kiasi kikubwa kupambana na usugu wa madawa kwa mteja wetu’’

Akizungumzia uwekezaji mwingine,Nanyanga ameongeza kuwa  mbali na hayo lakini pia sasa wana uwezo wa kutoa vipimo vya aleji,ambapo kwa kiasi kikubwa jamii inasumbuliwa na aleji tofautitofauti zikiwemo za vumbi,vyakula na vingine tofauti ambapo mteja anaweza kugundua aleji yake imesababishwa na nini.

‘’Tunauwezo wa kupima parameta 20 tofauti za aleji vikiwemo vyakula vya ngano na vingine’’anaeleza Nanyanga

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Upasuaji na Daktari Bingwa wa Mifupa na Majeraha katika hospitali hiyo,Dk Lameck Moses amesema hivi karibuni wameongezewa huduma zingine katika ufanyaji wa upasuaji wa mifupa ikiwemo mifupa mirefu ya paja na ile ya chini ya goti.

Amesema Serikali imeongeza kasi ya uwekezaji katika hospitali hiyo ambapo kwa sasa mgonjwa haitaji kupata rufaa ili aweze kupata huduma za kibingwa kutoka kwa madaktari bingwa.

 

Mkuu wa Kitengo cha Upasuaji na Daktari Bingwa wa Mifupa na Majeraha katika hospitali hiyo,Dk Lameck Moses akizungumza na waandishi wa habari Oktoba 28,2024 (hawapo pichani) kuhusu Serikali ilivyoimarisha kitengo hicho ambapo kwa sasa wagonjwa hawaitaji rufaa ili kufika hapo kutibiwa

‘’Huduma za mifupa ambazo tunatoa za kibingwa ni zile za maumivu ya mifupa,maumivu ya viungio mbalimbali,huduma za kuvunjika au kupata majeraha mbalimbali ambayo yanatokana na aina mbalimbali za ajali hususani zile za barabarani na zile zinazotokana na mtu kujikata au kudondokewa na vitu au kuanguka mwenyewe wakati anatembea.

‘’Hivi karibuni tumeongezewa huduma mbalimbali ambapo mwanzoni  baadhi ya mivunjiko au majeraha tu ndio tulikuwa tunahudumia lakini kwa uwekezaji mkubwa wa Serikali na baadhi ya vifaa ambavyo hospitali imewekeza imeongeza chachu ya mivunjiko mbalimbali katika ufanyaji wa oparesheni hasa upasuaji wa mifupa’’amesema Dk Moses

‘’Tunawaasa wananchi waendele kufika katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini kwa sababu hadi sasa hivi hatuhitaji uwe na rufaa ndipo uje ufanye huduma za kibingwa za madaktari bingwa wa mifupa na unaweza ukatokea tu nyumbani na ukafika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini na kisha ukamuona Daktari Bingwa wa upasuaji wa mifupa na akakupatia huduma kwa muda mfupi zaidi kama Serikali inavyoelekeza’’amesema Dk.Moses

Baadhi ya wananchi waliofika kupata huduma katika hospitali hiyo wameeleza kufurahishwa kwao na kuishukuru Serikali ambapo uwepo wa huduma bora na za kisasa wanazopatiwa kwa utaratibu  maalum na kwa wakati  kumewafanya kujiona kama sio wagonjwa.

 

Mashine mpya za kisasa zilizopo ndani ya maabara ya hospitali hiyo

Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini Mtwara ilianza kazi Oktoba Mosi,2021 ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan  aliifungua rasmi mnamo Septemba 15,2023

 

Next Post
VETA yaanzisha kozi kwa wafanyakazi wa majumbani (house girl/boy)

VETA yaanzisha kozi kwa wafanyakazi wa majumbani (house girl/boy)

VETA yawakaribisha wastaafu kujifunza masomo ya ufundi stadi

VETA yawakaribisha wastaafu kujifunza masomo ya ufundi stadi

DCEA:Raia wa nchi jirani wanafadhili kilimo cha bangi Mara,yakamata tani 7.8

DCEA yamkamata ‘papa’ mwingine wa biashara ya dawa za kulevya

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In