NA GOODLUCK HONGO,MTWARA
MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imewakaribisha watu waliostaafu katika utumishi wao wa kazi kujiunga na mafunzo ya ufundi ili kuweza kuwapatia ujuzi pamoja na ujasiria mali wa kuweza kujiendeshe Maisha ya kustaafu
Kauli ya VETA imekuja wakati ambapo baadhi ya wastaafu wameanza kujiunga na baadhi ya kozi zinazotolewa na chuo hicho huku wengine wakihamasika kutaka kujiunga ili kupata mafunzo ya ufundi stadi.
Kwa kudhihirisha hayo Bajeti Communication imefanya mazungumzo na mwanafunzi ambaye ni mstaafu anayesomea mafunzo ya mapishi mwaka wa pili Ester Mtumo ambaye ameeleza kujisikia furaha na amani kwani yeye amekuwa na ujuzi ambao utamsaidia kwenda kusimamia kazi zake pamoja kujipatia kipato.
Mtumo amebainisha kuwa aliamua kusomea fani hiyo baada ya kustaafu akiwa mtumishi wa umma na kisha kukaa nyumbani bila kazi.
‘’Kwa wastafu wenzangu mafunzo ya ufundi hayabagui umri pamoja na umri wangu VETA wameweza kunifundisha ujuzi na nitaenda kuwa balozi mzuri kwa kufungua mradi wangu na kusimania.
‘’Hivyo ni muhimu kwa wastafu kufika VETA na kuchagua ujuzi ambao unaweza kumsaidia kuendesha maisha ya kila siku na kuondoka na adha zisizo za lazima”amesema Mtumo

Amesema VETA ina fursa nyingi inazozitoa kupitia kozi zake zikiwemo za kupaka rangi,useremala na nyingine ambapo mtoto anaweza kusoma hadi chuo kikuu lakini akakosa mafunzo ya ufundi stadi ambayo yanaweza kumsaidia sana.
‘’Wengi wananiuliza kwa umri wangu huu kwanini nasomea mapishi lakini katika kozi yangu hii niliyoanza 2023 na nitahitimu mwezi Desemba nimejifunza mambo mengi sana na nimegundua makosa mengi sana.
‘’Elimu haina mwisho na mtu anaweza kusoma hata akiwa mzee na akafanya vizuri na mimi nafanya hivyo kivitendo na natarajia baada ya kumaliza kozi yangu hii nitafungua bekari yangu ambapo naweza kuoka mikate na vitu vingine vingi’’amesema Ntumo
Ntumo ameongeza kuwa VETA kuna fani nyingi za watu wanaokaa nyumbani hivyo ni muhimu wakafika kupata ujuzi kwani hata baadhi ya walimu waliostaafu kwa sasa nao wanataka kujiunga na chuo baada yeye kuchua hatua hiyo
Mfumo huo wa kuwafundisha ujasilimali watu waliostaafu utumishi wao unaweza kuliokoa kundi hilo ambao wengi wao wanategemea kuishi kwa kiinua mgongo(Pension) hali inayowapeleka kuishi maisha magumu na ya kuhangaika.
Akizungumza na Bajeti Communication Oktoba 28,2024 mkoani Mtwara,Mkuu wa Chuo cha VETA mkoani humo Theresia Ibrahim amesema Rais Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa kila wilaya kunakuwa na Chuo cha VETA ili kutoa mafunzo ya ufundi stadi kwani hakuna maendeleo bila mafundi.

Amesema chuo kinaandaa mafundi ambao ni mahiri wanaoweza kujiari na kuajiriwa pamoja na kuwajiri wengine ,ikiwemo kushiriki kwenye kazi za maendeleo katika wilaya wana zotoka mfano ujenzi wa hospitali, shule na miradi mingine.
Ibrahim amefafanuwa kuwa elimu ya mafunzo ya ufundi stadi hailengi watu,kundi wala kada fulani bali ni mafunzo ya watu wote ili mradi ahitaji mafunzo
”Mtanzania aliyestaafu tuna mpatia frusa hapa kwetu VETA-Mtwara ya kumfundisha ujuzi mdogo mdogo ambao anaweza kujishulisha akiwa nyumbani kwake pamoja na mafunzo mjasiriamali ili kuwasaidia wastaafu hawa kusimamia pesa waliopata kama pension kuendesha na kusimamia miradi midogo midogo kijasiriamali na endapo mstaafu atajishughulisha ni moja ya mazoezi na kujipatia kipato pia.
‘’Tuna kozi za muda mrefu na mfupi zikiwemo za udereva wa malori na mabasi ya abiria na ya watu binafsi,kozi za viyoyozi na majokofu,tunafundisha uzalendo hasa kwa bodaboda,na sisi hapa tuna hoteli yetu ya VETA hivyo nayo inatumika kuwafundisha wanafunzi wetu
‘’Tunaanzisha mfumo wa kukaa na watoto wa kike hadi wafikie malengo yao,tunaruhusu pia mafundi wenye ujuzi wao kurasimisha ujuzi wao,tunafundisha pia ujasiriamali lakini pamoja na kutoa mafunzo,tunatoa pia na huduma ya malazi kupitia hoteli yetu ya VETA-Mtwara’’amesema Ibrahim
Naye Mwalimu anayefundisha Kozi ya Food Producation Felister Shirima amesema wanafundisha pia kutengeneza vyakula vya asili vya kitanzania na vyakula kutoka mabara yote duniani

‘’Watu wa mabara mengine wanaweza kupata chakula cha asili yao lakini pia sisi VETA-Mtwara tunafundisha jinsi ya kutengeneza vitafunwa pamoja na keki,biskuti,maandazi na mikate zikiwemo keki zinazotokana na zao la Mwani”ameongeza Shirima





Discussion about this post