• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

DCEA yamkamata ‘papa’ mwingine wa biashara ya dawa za kulevya

Ni miezi miwili imepita tangu kukamatwa kwa wakala wa dawa za kulevya nchini

by bajeti
November 13, 2024
in Habari
0
DCEA:Raia wa nchi jirani wanafadhili kilimo cha bangi Mara,yakamata tani 7.8

Wananchi wa Wilaya ya Tarime mkoani Mara wakishiriki operesheni ya kutokomeza dawa za kulevya aina ya bangi iliyoendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dwa za Kulevya (DCEA) hivi karibuni(Picha na DCEA)

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini Tanzania (DCEA) imeendelea na jitihada zake za kulinda afya na usalama  wa watanzania kwa kuhakikisha kuwa tatizo la dawa za kulevya nchini linakomeshwa baada ya kumkamata kinara wa biashara hiyo jijini Dodoma.

Hata hivyo sio kazi rahisi kuwakamata ‘mapapa’ wa biashara hizo kutokana na kuwa na mtandao mkubwa wa ndani na nje ya nchi huku wakitumia teknolojia ya hali ya juu katika kufanikisha biashara zao ikiwemo fedha.

Taarifa za kukamatwa kwa anayetuhumiwa kuwa kinara wa biashara ya dawa za kulevya Mkoa wa Dodoma Suleiman   Mbarouk Suleiman maarufu kama ‘Nyanda’ ambaye alikuwa akifuatiliwa kwa muda mrefu bila kukamatwa zimetolewa jijini Dar es Salaam na Kamishna Jenerali wa DCEA Aretas Lyimo wakati akizungumza na waandishi wa habari Novemba 12,2024.

Kukamatwa kwa Nyanda kumekuja miezi miwili baada ya DCEA kumkamata Richard Mwanri anayetuhumiwa kuwa wakala wa dawa za kulevya nchini  ambaye amekuwa akipokea dawa hizo kutoka nchi mbalimbali duniani na kuziingiza nchini kwa usafiri wa magari zikiwa zimefichwa kwa kuchanganywa na bidhaa nyingine kisha kuzisambaza .

Akizungumzia kukamatwa kwa Nyanda,Kamishna Jenerali Lyimo amesema DCEA iliwakamata watuhumiwa wawili akiwemo Nyanda na Kimwaga Msobi Lazaro ambaye ni mkazi wa Mtaa wa Kinyali Kata ya Viwandani wakiwa na gramu 393 za dawa za kulevya aina ya heroin.

Amesema Nyanda anafahamika kama kinara wa biashara ya dawa za kulevya mkoani humo na amekuwa akifuatiliwa kwa muda mrefu kabla ya kukamatwa kwake akiwa na dawa hizo  za kulevya.

Kamishna Jenerali Lyimo amebainisha kuwa mafanikio hayo ni matokeo ya nia dhabiti ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan  la kuhakikisha kuwa tatizo la dawa za kulevya linakomeshwa ili kulinda afya na usalama wa watanzania.

Amesema mbali na Nyanda lakini pia wamewakamata watuhumiwa wengine 58 katika operesheni iliyofanyika maeneo mbalimbali nchini kuanzia Oktoba na Novemba 2024.

‘’Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imefanya operesheni katika maeneo mbalimbali nchini kati ya Oktoba na Novemba 2024 na kufanikiwa kukamata kilogram 1,066.105 za dawa za kulevya ,mililita 447 za dawa tiba zenye asili ya kulevya,na kuteketeza jumla ya ekari 157.4 za mashamba ya bangi na lita 19,804 za kemikali bashirifu.

‘’Uchunguzi umebaini kuwa wateja wengi wa skanka ni wanawake ,ambao hudai kutumia dawa hizo kupunguza msongo wa mawazo na kujistarehesha”amesema Kamishna Jenerali Lyimo

Skanka ni aina ya bangi ya kusindika yenye kiwango kikubwa cha kemikali yenye sumu aina ya Tetrahydrocannabinol (THC) ambayo inaweza kuharibu mfumo wa fahamu, akili na kusababisha magonjwa yasiyoambukiza kama vile moyo, figo, na ini.

Mbali na skanka lakini pia kuna hashish ambayo hutengenezwa kwa mchanganyiko wa maua na mafuta ya mbegu za bangi na inapovutwa huzalisha kemikali hatari zinazoweza kusababisha magonjwa ya akili kwa haraka na mara nyingi jamii huamini kuwa watu wanaopatwa na magonjwa haya wamerogwa.

‘’DCEA inaowamba wananchi kuendelea kuunga mkono jitihada hizi kwa kufichua wafanyabiashara wa dawa za kulevya na kuhamasishana kutoshiriki katika biashara na matumizi ya dawa za kulevya.’’amesema Kamshna Jenerali Lyimo

Awali Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Septemba 10,2024 Kamishna Jenerali Lyimo alieleza kuwa wataendela kufanya operesheni mashambani,barabarani na sehemu nyingine na kuwakamata wahusika ili kulinda afya za watanzania.

Next Post
TFRA yapokea matokeo ya utafiti kuhusu uzalishaji wa mbolea kwa kutumia malighafi zinazopatikana nchini

TFRA yapokea matokeo ya utafiti kuhusu uzalishaji wa mbolea kwa kutumia malighafi zinazopatikana nchini

Maajabu kaburi la Chifu Manjonda linalopatikana katika Msitu wa Hifadhi ya Mazingira Asilia-Rondo

Maajabu kaburi la Chifu Manjonda linalopatikana katika Msitu wa Hifadhi ya Mazingira Asilia-Rondo

NHC kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi Mkoa wa Lindi kupitia Mradi wake wa  Mtanda Complex

NHC kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi Mkoa wa Lindi kupitia Mradi wake wa Mtanda Complex

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In