• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Ajali iliyohusisha Bajaji yauwa watu watano Songwe

by bajeti
November 23, 2024
in Habari
0
Ajali iliyohusisha Bajaji yauwa watu watano Songwe

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe SACP- Augustino Senga

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,SONGWE

JESHI la Polisi Mkoa wa Songwe limethibitisha kutokea kwa ajali ya barabarani iliyohusisha gari T. 958 BCS aina ya Scania na Bajaji yenye namba MC. 783 DUF aina ya TVS na kusababisha vifo vya watu watano.

Ajali hiyo imetokea Novemba 22, 2024 majira ya saa 3:15 usiku ambapo bajaji hiyo ilikuwa ikitokea barabara ya Mji mdogo wa Mpemba na kuelekea Mji wa Tunduma na kujaribu kuyapita magari mengine yaliyokuwa mbele yake kisha kugongana na gari hilo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Novemba 23,2024 na  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe SACP- Augustino Senga amesema Bajaji hiyo ilikuwa ikiendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina la Emmanuel Hakimu Kalinga Mkazi wa Muungano Mjini Tunduma na kusababisha vifo vya watu watano  akiwemo dereva wa Bajaji hiyo.

Kamanda Senga amewataja waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni, Emmanuel Hakim Kalinga ambaye alikuwa Dereva wa Bajaji, Rehema Christopher  Sikamnga, (25) na mkazi wa Msongwa, Festo Aron Mambwe (57) Mkristo Msafwa mkazi wa Mbeya, Rosemary Njema (44) mkazi wa Ipito Tunduma na Milembe Siyantemi (36) mkazi wa Kapele.

Marehemu hao wamehifadhiwa katika Kituo cha Afya Tunduma kilichopo Wilaya ya Momba na chanzo cha ajali hiyo bado kinachunguzwa ambapo  Dereva wa Scania anatafutwa.

”Jeshi la Polisi Mkoa Songwe linatoa wito kwa madereva na wamiliki wa vyombo vya moto kukagua vyombo vyao kabla ya kuanza safari na kuzingatia sheria za usalama barabarani wakati wote”amesema Kamanda Senga

Next Post
Makumi ya watu na raia wa kigeni wamiminika kuangalia maajabu ya Mti wa Mwalimu Nyerere

Makumi ya watu na raia wa kigeni wamiminika kuangalia maajabu ya Mti wa Mwalimu Nyerere

Kamishna Jenerali Lyimo:Serikali hairogwi hata siku moja,yakamata boti,magari na ‘kuwapukutisha mapapa ‘wa biashara ya dawa za kulevya

Kamishna Jenerali Lyimo:Serikali hairogwi hata siku moja,yakamata boti,magari na ‘kuwapukutisha mapapa ‘wa biashara ya dawa za kulevya

Uchaguzi Serikali za Mitaa,ni Tanzania pekee Makamu wa Rais anapanga foleni na wananchi kupiga kura

Uchaguzi Serikali za Mitaa,ni Tanzania pekee Makamu wa Rais anapanga foleni na wananchi kupiga kura

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:0
  • Today's page views 0
  • Total visitors 13,056
  • Total page views 14,801

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In