• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Siasa

CUF yaomba Uchaguzi Mkuu kuwa huru,haki na amani

yasema haiwezi kususia uchaguzi

by bajeti
July 3, 2025
in Siasa
0
CUF yaomba Uchaguzi Mkuu kuwa huru,haki na amani

Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba

Share on FacebookShare on Twitter

 

NA  MWANDISHI WETU,MTWARA

CHAMA Cha Wananchi (CUF) kimemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kuwa Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika miezi michache ijayo unakuwa huru,haki na amani.

CUF imetoa wito huo wakati kukiwa na vuguvugu la kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika miezi michache ijayo  wakati vyama vingine kikiwemo Chama cha Mapinduzi (CCM) kikiendelea na zoezi la kutoa fomu kwa wanachama wake kwa ajili ya nafasi za ubunge na udiwani kabla ya kupata mgombea mmoja wa nafasi hizo.

Akizungumza na Bajeti Communication mkoani Mtwara Julai 2,2025,Mkurugenzi wa Habari,Uenezi na Mahusiano kwa Umma  wa CUF Mhandisi Mohamed Ngulangwa amesema kwa sasa CUF inaendelea na mchakato wa ndani kwa ndani wa kutoa na kurudisha fomu kwa wanachama wake.

Amesema ifikapo Julai 15,2025 itakuwa ndio mwisho wa wanachama wao kuchukua na kurudisha fomu za kuomba kuteuliwa na chama hicho kugombea nafasi za ubunge na udiwani katika maeneo yote nchini.

“Sisi tutashiriki uchaguzi wala hatutasusia,kwani mwaka 2015 tulisusia uchaguzi wa marudio kule Zanzibar baada ya kufutwa uchaguzi wa kwanza  na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (ZEC) Jecha Salim Jecha.

“Tunamuomba Rais Samia Suluhu Hassan na vyombo vingine vinavyohusika na uchaguzi kuhakikisha kuwa uchaguzi unakuwa huru,haki na wa amani”amesema Mhandisi Ngulangwa

Mhandisi Ngulangwa amebainisha kuwa wao hawafanyi siasa za ‘lipstick’ kwamba kila kinachofanyika lazima kiwe wazi kwa vyombo vya habari lakini baada ya kumaliza zoezi lao la mchakato wa wa ndani wa kuwapata wagombea wao ndipo wataanza kuwatangaza rasmi.

Next Post
ZAFICO yatambulisha ufugaji wa samaki wa vizimba

ZAFICO yatambulisha ufugaji wa samaki wa vizimba

Mafanikio ya Miaka Minne ya Uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika Tasnia ya Mbolea Tanzania

Mafanikio ya Miaka Minne ya Uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika Tasnia ya Mbolea Tanzania

Mkutano Waganga Wakuu wa Mikoa na Hamlashauri

Mkutano Waganga Wakuu wa Mikoa na Hamlashauri

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In