NA MWANDISHI WETU,SONGWE
JESHI la Polisi Mkoa wa Songwe linaendelea na msako wa kumtafuta Exavery Mwaweza kwa tuhuma za kumjeruhi na kusababisha kifo cha Evaristo Mwambogolo mkazi wa Wilaya na Mbozi
Mwaweza anadaiwa kumchoma kisu kifuani Mwambogolo baada ya kile kilichoelezwa kuwa ni ya mabishano ya mpira wa miguu kati ya timu za Simba na Yanga.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Septemba 17,2025 kwa vyombo vya habari na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe SACP Augustino Senga amesema tukio la mauaji hayo lilitokea mnamo Septemba 16,2025 saa 12:50 jioni katika Kitongoji cha Ululu,Kijiji na Kata ya Idiwili wilayani Mbozi Mkoa wa Songwe
Amesema katika tukio hilo,Evaristo Mwambogolo mkazi wa Ululu wilayani Mbozi alichomwa kisu kifuani,eneo la moyo na mtu aliyefahamika kwa jina la Exavery Mwaweza baada ya mabishani ya mpira wa miguu kati ya timu za Simba na Yanga
“Marehemu alijeruhiwa vibaya na alifariki dunia akiwa njiani akipelekwa kwenye Zahanati ya Iyula iliyopo Wilaya ya Mbozi kwa ajili ya matibabu.
“Uchunguzi wa awali umeonesha kuwa chanzo cha tukio hilo ni ushabiki wa mpira wa timu ya Simba na Yanga kati ya marehemu na mtuhumiwa,ambapo mtuhumiwa alitumia kisi alichokuwa nacho wakati wa ugomvi huo na mara baada ya kutenda kosa hilo alitoroka kusikojulikana”amesema Kamanda Senga
Kamanda Senga amebainisha kjuwa Jeshi la Polisi linaendelea na msako mkali wa kumtafuta mtuhumiwa huyo ili akamatwe na aweze kuhukumiwa kwa mujibu wa sharia
“Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe linatoa wito kwa wananchi kuepuka kujichukulia sheria mkononi,na kutojihusisha na vitendo vya vurugu vinavyoweza kusababisha madhara makubwa ikiwa ni pamoja na upotevu wa maisha.
“Jeshi la Polisi linawataka wananachi kuendelea kudumisha amani,mshikamano na utulivu,hasa wakati wa mijadala au mabishano ya kawaida ikiwemo michezo”ameongeza Kamanda Senga




Discussion about this post