• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Serikali ya ADA-TADEA kuwalipa askari walioshiriki vita vya Kagera

Wasema hawakustahili kulipwa 5,000

by bajeti
September 22, 2025
in Habari
0
Serikali ya ADA-TADEA kuwalipa askari walioshiriki vita vya Kagera

Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Cha African Democratic Alliance(ADA-TADEA) Georges Bussungu

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

CHAMA Cha African Democratic Alliance(ADA-TADEA) kimeeleza kuwa kitawalipa askari wote walioshiriki vita vya Kagera kiasi cha Sh.Milioni saba kila mmoja endapo kitachaguliwa na wananchi kushika dola katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29,2025.

Mbali na hilo lakini pia kitaunda chombo madhubuti kinachojitegemea na chenye uwezo  wa kufanya kazi za kijasusi duniani ikiwemo pia Taasisi ya Upelelezi Tanzania (TUTA).

Hayo yamebainika ndani ya Ilani ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025-2030 ya chama hicho  iliyozinduliwa Septemba 14,2025 Mbagala mkoani Dar es Salaam muda mfupi baada ya kuzindua kampeni za urais,ubunge na udiwani ili kuwanadai wagombea wao nchi nzima.

Ilani hiyo yenye kauli mbiu “Uhuru na Uwajibikaji, Tanzania Mpya yenye Utajiri wa Haki na Amani”imeeleza kuwa katika suala la  mabadiliko ya ulinzi na usalama  wao hawana Mjomba wala Shangazi wa kuwaonea huruma au kuwabeba bali ni wao wenyewe kujisimamia.

Ilani hiyo imebainisha  kuwa ili kuwa salama inabidi kuangalia masuala matatu ambayo ni Usalama wa Taifa ,Jeshi la Wananchi na Usalama wa Raia.

“Kitu cha msingi ambacho tutakifanya  ni kuwalipa askari wote walioshiriki vita vya Kagera ,sasa ni zaidi ya miaka 40 askari hao hawajalipwa.

“Cha kushangaza fedha zilitolewa ,inadaiwa kuwa walilipwa lakini wanajeshi wenyewe wanalalamika hadi leo,kwa sababu hakuna ushahidi  kama walilipwa au hakuna nyaraka zinazoonesha waliweka saini kupokea  malipo hayo ,tuna imani hawajalipwa .

“Hivyo sisi tutawalipa wote kutokana na ukweli kuwa orodha yao ambayo ipo,na watalipwa Shs.Milioni saba(7,000,000/=) kila mmoja badala ya Shs.Elfu tano(5,000/=) walizodaiwa kulipwa ,kwani walifanya kazi kubwa ya kizalendo kulipa ushindi Taifa letu”imebainisha Ilani hiyo

Aidha imeogeza kuwa itaunda chombo madhubuti kinachojitegemea na chenye uwezo mkubwa wa kufanya kazi za kijasusi duniani ambacho ni  Wakala wa Tanzania wa Ujasusi (WATU) Tanzania Agency for Intelligent (TAI)

Wafuasi wa Cha African Democratic Alliance(ADA-TADEA) wakimsikiliza mgombe wao Georges Bussungu wakati wa mikutano ya kampeni ya chama hicho Visiwani Zanzibar hivi karibuni

Hata hivyo chama hicho kupitia Ilani yake imejipanga kuhakikisha kuwa  itabadilisha mtazamo wa Jeshi la Polisi na Magereza  kuwa ni kujali utu na maslahi  ya wananchi zaidi ikiwemo kuunda Taasisi ya Upepelezi Tanzania(TUTA)-Bureau of Investigation ina Tanzania (BIT)

“Taasisi  hiyo itajitegemea tofauti na Polisi  ila itashirikiana na vyombo vingine  vya usalama,Polisi italazimika kuwa makini na rafiki wa raia ili iweze kufanya kazi zake vizuri.

“Iwe ni marufuku kwa Polisi kufanya unyanyasi kwa raia  na wanapaswa kuzingatia usalama wa Raia na Mali zao kwa kuheshimu utu na heshima za watu na haki za binadamu kwa mujibu wa sheria”imefafanuwa Ilani hiyo

Mwenyekiti wa ADA-TADEA  na mgombea wa urais Zanzibar Juma Ali Khatibu amesema kuwa Ilani ya chama chao imejiwekea mtanzamo maalum kwa upande wa Zanzibar

Amebainisha kuwa lengo kubwa ni kuendelea kuenzi Mapinduzi  Matukufu ya Zanzibar ,kuimarisha Muungano ili kujenga msingi imara wa kiuchumi  na siasa kwa kuthamini utamaduni,mila na desturi ili kuwa na Tanzania Mpya yenye utajiri,haki na amani.

“Nia yetu kuu ni kuwaunganisha wananchi ili washirikiane  kukuza uchumi wao binafsi na wa Taifa kwa ujumla.

“Kwa heshima ninawaomba kura zenu za NDIYO kwangu kama Mgombea wa  kiti cha Urais Zanzibar,Ndugu Georges Gabriel Bussungu ,Mgombea wa nafasi  ya Urais wa Jamhuri ya Muunganio wa Tanzania  na uwezo katika nafasi za Ubunge,Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi na Udiwani.

“ADA-TADEA itatumia fursa muhimu kwa Zanzibar kuwa na Utalii wa mikutano na kinachotakiwa baada ya sisi kuchaguliwa  ni kuweka miundombinu mizuri katika maeneo ya kufanyia mikutano hiyo”amesema Khatibu

Katibu Mkuu wa Chama hicho Salehe Msumari ameelezea ilani yao kuwa ni bora kuliko za vyama vingine  na kwamba ADA-TADEA kimekuwa na kuendeela kupanuka kutokana na hamu ya wananchi kujikomboa kutoka kwenye uchumi hodhi,utumwa wa fikra  za ukoloni mambo leo na nguvu ya ubeberu

“Chama hiki kiliundwa  kwa lengo la kuleta mabadiliko kawa amani ya kisiasa  nchini Tanzania  yaliyoongozwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Tanzania African National Union (TANU) na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  wakati wa awamu ya kwanza Hayati Oscar Salathiel Kambona(1925-1997)”amesema Msumari

Next Post
Safari ya mafanikio ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na miaka minne ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan

CCM kuwezesha ujenzi wa  nyumba 50,000 za makazi ya bei nafuu ifikapo 2030

ACT-Wazalendo kufanya kampeni nchi nzima Uchaguzi Serikali za Mitaa

ACT-Wazalendo kufanya uchunguzi huru wa matukio ya utekaji, utesaji, upoteaji na mauaji ya raia

Serikali ya ADA-TADEA kufuta upendeleo,rushwa na ufisadi

Serikali ya ADA-TADEA kufuta upendeleo,rushwa na ufisadi

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In