NA MWANDISHI WETU, GEITA
MGOMBEA nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Salum Mwalimu amesema hatma ya maisha ya watanzania ni Oktoba 29,2025 kuamua yabadilike au yabakie yalivyo.
Mwalimu ameyasema hayo Septemba 16,2025 mkoani Geita wakati akiwahutubia wakazi wa mji huo na kuwaomba kukichagua chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29,2025

“Hatima ya maisha yako 2025 , 2030 yapo mikononi mwako kuchagua yabadilike kiuchumi na kijamii au kuacha yaendelee yalivyo sasa,
“Geita kama ilivyo mikoa mingine yenye dhahabu nyingi, lakini haina kielelezo chochote cha kuonyesha alama ya madini hayo,
“Ninawaomba sana hatima ya maisha yetu ni Oktoba 29 mwaka huu, nendeni mkaichague CHAUMMA iweze kuimarisha hali nzuri za maisha yenu,maana kama mna dhahabu na samaki wengi lakini hamna viwanda vya kuchakata haina maana” amesema Mwalimu

.Hata hivyo amebainisha kuwa CHAUMMA kipo tayari kupamba na umaskini wa watanzania lakini pia kuandika Katiba Mpya.




Discussion about this post