• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Friday, May 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

GEF kuendelea kufadhili miradi ya mazingira

by bajeti
February 20, 2023
in Mazingira
0
GEF kuendelea kufadhili miradi ya mazingira

Afisa Mazingira wa Mabadiliko ya Tabianchi kutoka Mfuko wa Mazingira wa Dunia (GEF) Filippo Berarch akitazama mbegu za alizeti zinazotumika kwa ajili ya kutengeneza mafuta na mashudu ya vyakula vya mifugo wakati wa ziara ya ujumbe huo kukagua Mradi wa Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia Mifumo Ikolojia (EBARR) unaotekelezwa na kusimamiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais wakati wa ziara ya ujumbe huo Februari 15, 2023 wilayani Mpwapwa Mkoa wa Dodoma.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,DODOMA

MFUKO wa Mazingira wa Duniani (GEF) umesema utaendelea kufadhili miradi ya mazingira inayozunguka jamii nchini ili kuongeza kasi ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira katika maeneo ya vijijini

Hata hivyo GEF  itahakikisha jamii inajishughulisha na kilimo rafiki kwa mazingira na kutolea mfano kilimo cha mbogamboga.

Hayo yamejitokeza baada ya mfuko huo kuridhishwa na utekelezaji wa Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia Mifumo Ikolojia (EBARR) unaotekelezwa katika Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma na kusimamiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais.

GEF imetoa kauli hiyo Februari 15, 2022 kupitia ujumbe wa Mfuko huo ukiongozwa na Mratibu wake Kanda ya Afrika, Dkt. Ibrahima Sow wakati wa ziara ya kutembelea Mradi huo katika Vijiji vinne vya Wilaya hiyo.

Dkt. Sow amesema GEF imedhirishwa na utekelezaji wa miradi hiyo ambayo ni ujenzi wa visima virefu vinne, malambo mawili, majosho mawili, vitalu nyumba vitatu na mashine ya kukamulia alizeti ambapo miradi hiyo imeweza kuwa chanzo mbadala cha kuongeza kipato kwa wananchi.

“GEF itaendelea kufadhili miradi ya mazingira inayozunguka jamii ili kuongeza kasi ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira katika maeneo ya vijijini sambamba kuhakikisha jamii inajishughulisha na kilimo rafiki kwa mazingira na kutolea mfano kilimo cha mbogamboga.

“Miradi hii ina faida kubwa kwa wananchi wa Mpwapwa, natoa rai kwa jamii kuweza kuitunza na kuwasaidia kwa ajili ya kuleta manufaa ya sasa na kwa kizazi kijacho” amesema Dkt. Sow

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa EBBAR Kitaifa, Dkt. Makuru Nyalobi amewataka wananchi wa Wilaya hiyo kusimamia vyema miradi hiyo ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao ambayo inatarajia kuwanufaisha wananchi wa vijiji vya Nghambi, Mbugani, Kiegea na Kazania.

Amebainisha  kuwa Mradi huo pia unatekelezwa katika Wilaya nyingine nne ambazo ni Kaskazini ‘A’ Unguja visiwani Zanzibar,Simanjiro mkoani Manyara, Mvomero Mkoa wa Morogoro na Kishapu mkoani Shinyanga

Aidha ameongeza kuwa miradi hiyo imetekelezwa kwa kutumia mifumo ikolojia ambapo mipango ya matumizi ya ardhi imeandaliwa.

Naye Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Mbugani, Aziza Mwinyimbweni amesema Serikali ya Kijiji hicho imejipanga katika kuhakikisha kuwa mradi huo unafikia malengo yaliyowekwa na Serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii ikiwemo maji safi na salama.

Next Post
Putin:Kuishinda Urusi ni jambo lisilowezekana

Putin:Kuishinda Urusi ni jambo lisilowezekana

Vumbi laitesa Cameroon

CCM yawaonya wafanyabishara,wawekezaji wanaokwepa kodi

CCM yawaonya wafanyabishara,wawekezaji wanaokwepa kodi

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:0
  • Today's page views 0
  • Total visitors 16,333
  • Total page views 18,523

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In