• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Putin:Kuishinda Urusi ni jambo lisilowezekana

by bajeti
February 21, 2023
in Habari
0
Putin:Kuishinda Urusi ni jambo lisilowezekana

Rais Vladmir Putin wa Urusi

Share on FacebookShare on Twitter

MOSCOW,URUSI

RAIS wa Urusi Vlamidir Putin amesema kuishinda Urusi katika kile inachoeleza kuwa ni oparesheni ya kijeshi iliyoianzisha nchini Ukraine ni jambo lisilowezekana.

Kauli ya Rais Putin inakuja wakati ambapo Rais wa Marekani Joe  Biden akifanya ziara ya kushtukiza na kukutana na Rais wa Ukraine Volodimir Zelensky na kuahidi kuipatia msaada zaidi wa kijeshi ili kuishinda Urusi baada ya kuanzisha oparesheni ya kijeshi Februari 24,2022.

Akizungumza  wakati wa hotuba ya kila mwaka ya hali ya taifa mbele ya mabaraza yote mawili ya bunge na makamanda wa kijeshi  Februari 21,2023 jijini Moscow,Rais Putin  amesema Moscow itatekeleza kwa ustadi mipango ya kijeshi na kutimiza malengo yake nchini Ukraine na nchi  za Magharibi zinawajibika kubeba dhamana kikamilifu juu ya vita hivyo.

Amesema  Urusi itaendelea  na vita nchini Ukraine na kuyaonya  mataifa ya nchi za magharibi zinazoongozwa na Marekani  kuwa yanauchochea zaidi mzozo uliopo kwa mataumini ya kuishinda Urusi.

Amesema Urus i ilifanya kila inaloweza kuepusha vita lakini Ukraine ikiungwa mkono na mataifa ya magharibi ilikuwa inapanga njama za kuivamia rasi ya Crimea, eneo ambalo Moscow ililinyakua kutoka  Ukraine  mwaka 2014.

Rais Putin ameongeza kuwa  nchi za Magharibi bado zinaendelea kumimina fedha kuunga mkono vita na nchi hizo zilianza kuifanya Ukraine kuwa mpinzani wa Urusi muda mrefu.

Nchi za Magaharibi zikiongozwa na Marekani zimekuwa zikitoa msaada mkubwa wa kijeshi kwa Ukraine ili iweze kujilinda na mashambulizi ya Urusi lakini hali imekuwa tofauti baada ya Urusi kuendeleza mashambulizi makubwa katika nchi hiyo iliyo katikati mwa Bara la Ulaya huku ikiviweka tayari vikosi vyake vya silaha za nyuklia kwa mashambulizi ikiwa usalama wake kutokana na misaada ya nchi za magharibi itahatarisha usalama wake.

Next Post

Vumbi laitesa Cameroon

CCM yawaonya wafanyabishara,wawekezaji wanaokwepa kodi

CCM yawaonya wafanyabishara,wawekezaji wanaokwepa kodi

Boeing yasitisha  ndege za Dreamliner -787

Boeing yasitisha ndege za Dreamliner -787

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:5
  • Today's page views 5
  • Total visitors 13,061
  • Total page views 14,806

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In