• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Wednesday, May 6, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Jeshi la Polisi:Kutoa taarifa za uongo kwa nia ya kuihadaa jamii na kuiaminisha,ni kiashiria tosha cha kuvuruga amani, utulivu na usalama wa nchi yetu

by bajeti
November 28, 2024
in Habari
0
Jeshi la Polisi Tanzania laonya watumiaji mitandao ya kijamii

Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania DCP David Misime

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,DODOMA

JESHI la Polisi nchini limetoa wito kwa baadhi ya Viongozi wenye taarifa za kufanyiwa uhalifu wowote wa kijinai waziwasilishe kupitia taratibu zilizopo za kisheria na kujiepusha kuandaa taarifa za uzushi na za uongo kwa nia ya kuihadaa na kuiaminisha jamii kwa  mambo ambayo hayapo

Jeshi hilo limeongeza kuwa kuandaa taarufa za uzushi na za uongo ni kiashiria tosha kuwa, lengo lao si kujenga bali ni kutaka kuvuruga amani, utulivu na usalama wa nchi yetu.

Kauli ya Jeshi la Polisi imetolewa baada ya kusambaa kwa taarifa mbalimbali katika mitandao ya kijamii kuhusu matukio yaliyojitokeza wakati wa kufanyika kwa Uchaguzi  wa Serikali za Mitaa uliofanyika Novemba 27,2024 nchini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Makao Makuu ya Jeshi la Polisi  Novemba 28,2024 jijini Dodoma na Msemaji wa Jeshi la hilo nchini DCP David Misime amesema zipo taarifa kwenye Mitandao ya Kijamii na Vyombo vingine inayoonyesha kutolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Katavi, Roda Kunchela ikieleza kuwa, Mgombea wa Mtaa wa Miembeni Kilimahewa kupitia Chama hicho, Nsajigwa Mwandembwa alikamatwa na Polisi akiwa nyumbani kwake.

Aidha, ameeleza kuwa, huko katika eneo la Mwamkulu,Herman Lutambi Mzee amepigwa hadi kivunjwa mkono na Diwani wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Pia katika taarifa hiyo ameeleza kuna gari ndogo iliyotaka kumteka Christopher Kapaso aliyekuwa anagombea nafasi ya uenyekiti mtaa wa Kigamboni.

DCP Misime amebainisha kuwa Jeshi la Polisi limefuatilia kwa kina ukweli wa taarifa hizo ili ikibainika ni za kweli hatua za kisheria zichukuliwe.

‘’Baada ya ufuatiliaji huo sambamba na kuchukuwa maelezo ya watu mbalimbali, imebainika taarifa hizo ni za kutengeneza na  kuongeza chumvi ili kudanganya na  kupata huruma ya wananchi.

‘’Ukweli uliopo kulingana na watu walioshuhudia ni kwamba Nsagigwa Mwandembwa mgombea kiti cha Mtaa wa  Miembeni Kilimahewa alikuwa akifanya fujo kwenye kituo cha kupigia kura cha Miembeni na alionywa mara kadhaa lakini hakusikia.

‘’Baada ya kufikia hatua ambayo haivumiliki tena alikamatwa akiwa kwenye hicho kituo na kupelekwa kituo cha Polisi na kuhojiwa na bàada ya mahojiano na alipoona yeye mwenye athari ya vitendo vyake alidhaminiwa ili akakamilishe taratibu zake za uchaguzi kusubiri hatua zingine za kisheria.

DCP Misime ameongeza kuwa kuhusiana na taarifa aliyotoa kuwa, Herman  Lutambi Mzee amepigwa na Diwani wa CCM hadi kuvunjwa mkono, ufuatiliaji wa kina umefanyika na imebainika kuwa, kilichokuwepo ni mzozo baina yao kulikosababisha kuchaniana shati na wala hajavunjwa mkono kama Mwenyekitin alivyosema

‘’Kuhusu taarifa kuwa kulikuwa na jaribio la kumteka Christopher Kapaso, taarifa hizo zimefuatiliwa na hazina ukweli wowote.

‘’Jeshi la Polisi nchini lingependa kutoa wito kwa baadhi ya Viongozi kama wana taarifa za kweli kufanyiwa uhalifu wowote wa kijinai waziwasilishe kupitia taratibu zilizopo za kisheria na kujiepusha kuandaa taarifa za uzushi na za uongo kwa nia ya kuihadaa na kuiaminisha jamii mambo ambayo hayapo kwani ni kiashiria tosha kuwa, lengo lao si kujenga bali ni kutaka kuvuruga amani, utulivu na usalama wa nchi yetu’’amesema DCP Misime

Next Post

Shilingi ya Tanzania yaimarika dhidi ya dola ya Marekani

Karibu Tanzania Rais Joe Biden wa Marekani

Karibu Tanzania Rais Joe Biden wa Marekani

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari aungana na Rais Dkt.Samia kuadhimisha Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari aungana na Rais Dkt.Samia kuadhimisha Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:13
  • Today's page views 17
  • Total visitors 16,092
  • Total page views 18,257

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In