NA GOODLUCK HONGO
MWANASHERIA Mkuu wa Serikali Hamza Johari ameuangana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kuadhimisha miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara.
Tanzania inaadhimisha miaka 63 ya Uhuru ikiwa imeongozwa na marais sita akiwemo Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere,Hayati Ali Hassan Mwinyi,Hayati Benjamin William Mkapa,Dkt Jakaya Kikwete,Hayati John Pombe Magufuli na Rais wa sita Dkt.Samia Suluhu Hassan.
Katika kipindi chote cha Uongozi wa Viongozi hao Tanzania imebaki kuwa nchi pekee duniani yenye amani na utulivu jambo ambalo ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa.
‘’Mwanasheria Mkuu wa Serikali ,Mh.Hamza Johari kwa niaba ya Menejimenti na Watumishi wote wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ,tunaungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dkt.Samia Suluhu Hassan na Watanzania wote katika Maadhimisho ya Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara.
‘’Uongozi Madhubuti na Ushirikishwaji wa Wananchi ni Msingi wa Maendeleo yetu’’amesema Johari
Tanzania inajivunia misingi bora ya uongozi iliyowekwa na waasisi wa Taifa akiwemo Mwalimu Julius Nyerere kwa kuondoa ukabila,udini ikiwemo lugha ya Kiswahili kama lugha ya Taifa ambapo uongozi umekuwa ni wa kupokezana kila baada ya miaka mitano na 10.
Mfumo huo umesaidia katika kuhakikisha kuwa watanzania wanaishi kama ndugu hivyo kudumisha amani na utulivu.
Tanzania Bara ilipata uhuru wake Desemba 9,1961 wakati huo ikiitwa Tanganyika kutoka kwa wakoloni Waingereza ambapo Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliongoza mapambano ya kupata uhuru akiwa na Chama cha TANU na kuwa Waziri Mkuu wa kwanza kabla ya kuwa Rais wa Kwanza Tanzania Bara.
Aprili 26,1964 Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika iliungana na Zanzibar iliyokuwa ikiongozwa na Hayati Abeid Aman Karume na kuzaliwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania




Discussion about this post