• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Kamishna Jenerali Lyimo:Tutateketeza dawa za kulevya nchi nzima

Wateketeza kilogramu 614.12 za Dawa za kulevya mkoani Dar es Salaam ikiwemo heroin

by bajeti
December 21, 2024
in Habari
0
Kamishna Jenerali Lyimo:Tutateketeza dawa za kulevya nchi nzima

Wafanyakazi wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa a Kulevya (DCEA) wakishiriki zoezi la uteketezaji wa dawa hizo katika Kiwanda cha Saruji cha Twiga kilichopo Wazo mkoani Dar es Salaam Desemba 19,2024.

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imesema zoezi la uteketezaji wa dawa za kulevya walizozikamata litaendelea nchi nzima, kadri mahakama zitakavyoendelea kutoa amri

Kauli hiyo imetolewa Desemba 19,2024 mkoani Dar es Salaam na Kamishna Jenerali wa Mamlaka hiyo Aretas Lyimo wakati akisimamia zoezi la uteketeza wa  kilogramu 614.12 za dawa za kulevya  katika Kiwanda cha Saruji cha Twiga, kilichopo Wazo.

Wafanyakazi wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) wakishiriki zoezi la uteketezaji wa dawa hizo katika Kiwanda cha Saruji cha Twiga kilichopo Wazo mkoani Dar es Salaam Desemba 19,2024

Kuteketezwa kwa dawa hizo ni muendelezo wa kazi kubwa inayofanywa na DCEA katika kupambana na biashara hiyo yenye madhara makubwa kwa afya za watanzania na kiuchumi  .

Wafanyakazi wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) wakishiriki zoezi la uteketezaji wa dawa hizo katika Kiwanda cha Saruji cha Twiga kilichopo Wazo mkoani Dar es Salaam Desemba 19,2024

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uteketezaji wa dawa hizo, Kamishna Jenerali  Lyimo amesema , kati ya dawa zilizoteketezwa, kilogramu 601.87 ni methamphetamine na kilogramu 12.25 ni heroin ambapo dawa hizo zilikuwa zinashikiliwa kama vielelezo.

Amesema uteketezaji huo umefanyika baada ya Mahakama za Hakimu Mkazi Kibaha mkoani Pwani na Mahakama ya Hakimu Mkazi  Kisutu jijini Dar es Salaam kuamuru uteketezaji wake kutokana na hatari ya kuharibika au kubadilika umbo wakati kesi husika bado zinaendelea.

“Uteketezaji wa dawa hizi unafanyika kwa mujibu wa Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Namba 5 ya mwaka 2015 pamoja na Kanuni zake.

‘’Sheria hii inaruhusu uteketezaji wa dawa hizi kufanyika kabla, wakati, au baada ya shauri kumalizika mahakamani,” ameeleza Kamishna Jenerali Lyimo.

Wafanyakazi wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) wakishiriki zoezi la uteketezaji wa dawa hizo katika Kiwanda cha Saruji cha Twiga kilichopo Wazo mkoani Dar es Salaam Desemba 19,2024

Kamishna Jenerali Lyimo amebainisha kuwa uteketezaji huo unafanywa kwa njia zinazozingatia usalama wa afya ya watu na utunzaji wa mazingira, huku ukisimamiwa na wadau mbalimbali waliotajwa kisheria.

Aidha, Kamishna Lyimo ameongeza  kuwa katika mwezi huu wa Desemba pekee, Mamlaka imefanikiwa kuteketeza ekari 12 za mashamba ya bangi katika Mkoa wa Tabora, pamoja na kilogramu 398.105 za dawa mbalimbali mkoani Mtwara  na inatarajia kuteketeza kilo 126.21 za mirungi mkoani Arusha katika siku chache zijazo.

Dawa za Kulevya zikiwa katika maandalizi ya kuteketezwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) katika Kiwanda cha Saruji cha Twiga kilichopo Wazo mkoani Dar es Salaam Desemba 19,2024.

Kamishna amewapongeza wadau wote waliofanikisha uteketezaji wa dawa hizo na kuendelea kushirikiana na mamlaka katika juhudi za kupambana na biashara haramu ya dawa za kulevya na kuwa zoezi la uteketezaji litaendelea nchi nzima, kadri mahakama zitakavyoendelea kutoa amri.

“Tunaendelea kushirikiana na wadau kuhakikisha kuwa dawa hizi haramu zinadhibitiwa kwa ustawi wa jamii yetu,” amefafanuwa Kamishna Jenerali Lyimo.

Next Post
NHC Mkandarasi ‘Class A’anayejenga Majengo ya Wizara nane katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma

NHC Mkandarasi ‘Class A’anayejenga Majengo ya Wizara nane katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma

DCEA yazuia tani 159.3 za Kemikali Bashirifu kuingizwa nchini

DCEA yazuia tani 159.3 za Kemikali Bashirifu kuingizwa nchini

Miradi ya Iyumbu Nyumba 1000 na Medeli ilivyotatua changamoto ya makazi Dodoma

NHC yahimiza wapangaji kulipa kodi kwa wakati

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In